| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Waziri Mkuu wa zamani Kenya, Raila Odinga, 80, afariki
Kulingana na familia yake, Raila odinga amekuwa akipokea matibabu nchini India kwa siku kadhaa kabla ya habari za kifo chake kutangazwa mapema Jumatano.
Waziri Mkuu wa zamani Kenya, Raila Odinga, 80, afariki
Raila Odinga amefariki nchini India
15 Oktoba 2025

Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Kenya, Raila Odinga amefariki nchini India alipokuwa akipokea matibabu.

Raila anasifika kama mmoja wa viongozi wakongwe wa siasa nchini Kenya na anayefahamika kama mwanamageuzi.

Amekuwa nguzo muhimu katika siasa za nchi hiyo. Ana ushawishi mkubwa kwa wanaomuunga mkono na amekuwa na mchango mkubwa takriban katika kila serikali, licha ya yeye mara nyingi kuwa upande wa upinzani.

Wasifu wa Raila Odinga

Raila Amolo Odinga alizaliwa Januari 7 mwaka 1945. Amekulia katika mazingira ya siasa ambapo baba yake Mzee Jaramogi Oginga Odinga alikuwa mmoja wa wapigania uhuru wa Kenya na kuwa makamu wa kwanza wa Rais wa taifa hilo.

Alikuwa kwenye nafasi hiyo kwa kipindi cha chini ya miaka miwili. Raila Odinga pamoja na baba yake walikuwa miongoni mwa wanasiasa waliopigania kuwepo kwa siasa za vyama vingi katika miaka ya themanini na tisini

Raila aliwahi kufungwa gerezani kwa kuhamasisha kuwepo kwa vyama vingi vya kisiasa. Amegombea urais mwaka 1997, 2007, 2013, 2017 na 2022, kwa ujumla mara tano, ila hajapata fursa ya kuongoza taifa hilo la Afrika Mashariki, lakini amekuwa na mchango muhimu kwa kila serikali iliyokuwa madarakani.

Kabla ya uchaguzi wa mwaka 2002, chama cha Raila kilijiunga na serikali ya rais wa awamu ya pili Daniel Arap Moi na akawa Waziri wa Nishati.

Mwaka 2002 akasaidia upinzani ulioongozwa na rais wa awamu ya tatu Mwai Kibaki kupata ushindi mkubwa dhidi ya Uhuru Kenyatta na chama cha KANU.

Licha ya kuwa nje ya serikali, mchango wake bado ulionekana baada ya maandamano ya vijana maarufu Gen Z, mwaka 2024, ambapo alionekana kufanya tena ‘’handshake’’ na serikali ya Ruto, hatua iliyofanya baadhi ya viongozi wa upinzani kujumuishwa kwenye Baraza la Mawaziri.

Raila Odinga alimuoa mke wake Ida Odinga, mwaka 1973 n apamoja walijaaliwa watoto wanne.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti
Nigeria yaanzisha uchunguzi baada ya kukamata kilo 1,000 za kokeini yenye thamani ya $235M
Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam
Mtoto wa Gaddafi aachiliwa huru baada ya miaka kumi gerezani
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Zaidi ya mataifa 20 yanalaani ukatili wa RSF nchini Sudan, na kutaka kukomeshwa kwa ghasia
Rais wa Misri, afisa mkuu wa usalama wa Urusi kujadili ushirikiano wa kijeshi
Maelfu ya wananchi wanashikiliwa katika hali mbaya sana katika Al Fasher, Sudan: madaktari
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aghairi ziara iliyopangwa nchini Kenya
‘Mauaji ya waandamanaji ni chukizo mbele za Mungu’
Jeshi la Sudan lazima shambulio la RSF katika mji wa Babnousa huko Kordofan Magharibi
Majeshi ya Somalia yawaua viongozi watatu wakuu wa Al Shabaab
Rwanda, DRC zaanzisha mfumo wa ushirikiano wa kiuchumi huku kukiwa na mazungumzo ya amani
RSF yazika miili katika makaburi ya halaiki, inachoma wengine ili 'kuficha ushahidi wa mauaji
Wananchi katika Al Fasher, Sudan, wanakabiliwa na ukatili 'wa kiwango kisichoweza kuaminika' — UN
Chama tawala nchini Djibouti kimemteua Rais Guelleh kwa muhula wa sita
Amaan Golugwa akamatwa huku polisi Tanzania ikiwasaka viongozi wa upinzani kufuatia maandamano
Wafanyakazi waokolewa baada ya maharamia kushambulia meli ya mafuta kutoka Somalia