Daktari wa uzazi Australia ashtakiwa kufanya upasuaji usio sahihi na kuondoa viungo vya wanawake

'Kufanya upasuaji usio wa lazima ni kosa, kuondoa viungo vya mwanamke bila dharura ya kitabibu ni kosa na kusaidia kufanya hivyo pia ni kosa,' amesema Waziri Mkuu.

By
Mmoja wa wanawake aliondolewa mayai yake ya uzazi na mfuko wa uzazi lakini matokeo hayakuonesha dalili za ugonjwa huo. / AP

Daktari wa magonjwa ya uzazi kutoka Australia alipelekwa polisi Jumanne kutokana na madai ya vyombo vya habari kwamba alifanya upasuaji usiohitajika kwa wanawake, ikiwa ni pamoja na kutoa viungo.

Wagonjwa kadhaa wa daktari wa upasuaji wa Melbourne, Simon Gordon, walimwambia mtangazaji wa Shirika la Umma ABC kwamba aliwafanyia upasuaji kwa ajili ya maradhi makali licha ya ushahidi mdogo au kutokuwepo kwa ushahidi kwamba walikuwa na ugonjwa huo.

Baadhi yao waliisia kuugua kwa miezi au miaka baada ya taratibu hizo.

‘Endometriosis’ ni ugonjwa sugu ambao tishu zinazofanana na ukuta wa ndani wa mfuko wa uzazi huota nje ya mfuko wa uzazi.

Mmoja wa wanawake alitolewa mayai yake ya uzazi na mfuko wa uzazi lakini matokeo hayakuonesha dalili za ugonjwa huo, alisema mtangazaji.

Daktari mtaalamu wa upasuaji aliiambia ABC kwamba sampuli moja ilionyesha "idadi isiyo ya muhimu ya uwezekano wa endometriosis" kwa mgonjwa huyo na hakukuwa na sababu za kumtoa mfuko wa uzazi.

Mwanamke mwingine alisema daktari alimfanyia vipimo na kumfanyia upasuaji licha ya matokeo ya awali kutoonesha dalili za ugonjwa huo.

Miaka sita baada ya upasuaji, hakuweza kutembea kwa dakika tano bila maumivu.

"Hakuna ubora wa maisha ikilinganishwa na nilivyokuwa kabla," alinukuliwa akisema.

Gordon amekana kufanya makosa, akiiambia ABC kwamba hakuwahi kufanya upasuaji kwa ajili ya endometriosis "isipokuwa nilikuwa nimehakikishwa kabisa kwamba ilikuwa katika maslahi bora ya mgonjwa."

AFP imewasiliana na daktari huyo aliyekaribia kustaafu ili kupata jibu la tuhuma hizo.

Waziri Mkuu wa Australia Jacinta Allan alisema kuwa "amekuchukizwa" na madai hayo.

"Kufanya upasuaji usiohitajika ni uhalifu, kuondoa viungo vya mwanamke bila dharura ya kitabibu ni uhalifu na kusaidia katika kitendo hicho ni uhalifu," alisema katika taarifa.

Polisi wa jimbo la Victoria walisema walikuwa "wakitathmini taarifa."

ABC ilisema malalamiko kuhusu daktari huyo yalikuwa yamewasilishwa na wagonjwa na wataalamu wa afya kwa muda wa miaka mitano kwa Wakala wa Udhibiti wa Wataalamu wa Afya wa Australia.

Waziri Mkuu alisema Wakala wa Udhibiti anapaswa kuchukua malalamiko kwa uzito na kuchunguza kwa "muda unaofaa."

Mamlaka ya udhibiti ya Australia ilisema katika taarifa kwamba inatambua malalamiko ya wagonjwa hao na "inachunguza kikamilifu na kufanya tathmini.”