Waziri Mkuu wa zamani wa Burundi Jenerali Alain-Guillaume Bunyoni, ambaye alifungwa maisha gerezani kwa jaribio la mapinduzi, ameachiwa huru kwa misingi ya afya siku ya Jumatano, chanzo cha mahakama na jamaa yake kilielezea AFP.
Bunyoni alikuwa waziri mkuu kuanzia kati ya mwaka 2020 hadi Septemba 2022, wakati alipofutwa kazi, siku kadhaa baada ya Rais Evariste Ndayishimiye kuonya kuhusu madai ya mapinduzi dhidi yake.
Mashirika ya kutetea haki za binadamu yanasema kuwa maradhi yake ya kisukari yalizidi alipokuwa gerezani kutokana na kukosa matibabu na pia alikuwa na tatizo la mfumo wa neva.
Bunyoni, ambaye alikuwa mkuu wa polisi na waziri wa mambo ya ndani, alikuwa hospitali tangu Oktoba lakini "akaachiwa rasmi kwa muda kwa misingi ya afya," afisa huyo wa mahakama alisema kwa masharti asitambulishwe.
'Hali yake inatia wasiwasi'
Alipelekwa nyumbani kwake katika mji mkuu wa kibiashara wa Bujumbura.
"Hali yake inatiwa wasiwasi sana," jamaa yake mmoja aliiambia AFP, pia akizungumza kwa masharti ya kutotambulishwa.
















