| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Ghana yafanya uchunguzi wa kitaifa kuhusu madai ya plastiki katika chipsi za ndizi
Msimamizi alisema kuwa wanafanya kazi pamoja na mamlaka za ndani na Polisi wa Ghana ili kufuatilia wachuuzi.
Ghana yafanya uchunguzi wa kitaifa kuhusu madai ya plastiki katika chipsi za ndizi
Katika taarifa iliyotolewa na FDA, imesema uchunguzi ulilenga kubaini ukweli wa madai hayo na kuwalinda walaji. / Others
13 Machi 2026

Ghana imeanzisha uchunguzi wa kitaifa kuhusu tuhuma za kuchanganywa plastiki katika 'chips' za ndizi zinazouzwa nchini humo.

Mamlaka ya Chakula na Dawa (FDA) imesema imeanza kufuatilia bidhaa hiyo sokoni na kufanya vipimo vya maabara nchi nzima baada ya video iliysambaa katika mitandao ya kijamii inayoonesha waandaaji wa ndizi kwa makusudi wakiyeyusha plastiki katika mafuta ya moto wakati wa uandaaji kwa lengo la kuongeza wingi wa bidhaa hiyo lakini pia kurefusha muda wa kuharibika, kwa mujibu wa Wakala wa Habari Ghana.

Katika taarifa iliyotolewa na FDA, imesema uchunguzi ulilenga kubaini ukweli wa madai hayo na kuwalinda walaji.

"Kwa rekodi, kuyayusha plastiki kwa makusudi katika mafuta yanayochemka ni uharibifu wa moja kwa moja wa chakula, na kukifanya kutofaa kwa matumizi ya binadamu," imesema Mamlaka hiyo.

FDA imeonya kwamba bidhaa za plastiki, hasa mifuko katika mafuta ya moto, ni hatari kwa afya na kutoa sumu iliyopo kwenye plastiki na kuingia kwenye chakula," imesema.

Mamlaka imesema inashirikiana na mamlaka ya ndani na Polisi wa Ghana kufuatilia wachuuzi wanaoshukiwa na kuahidi kutoa matokeo ya uchunguzi pindi yatakapokamilika.

Kesi za chakula kuwa na sumu zimekuwepo siku za nyuma na zimehusishwa na chakula cha barabarani, maji machafu na kutokuwepo kwa sheria madhubuti.

Mwaka 2022, FDA ilifunga mgahawa maarufu baada ya kuwepo kwa taarifa za wateja kula chakula chenye madhara.

Soma zaidi
Watu kumi na nne waliotekwa Nigeria waokolewa: Gavana wa Jimbo
Ziara ya Afrika: Papa Leo afanya Misa nchini Angola
Wamefukuzwa Sahel: Ufaransa inatafuta nini nchini Kenya?
Pande zinazopigana DR Congo zimekubaliana kubadilishana wafungwa na kuruhusu ufikiaji wa msaada
Nigeria yavamia ‘kiwanda cha watoto’ huko Lagos, na kuwaokoa wanawake wajawazito
Marekani yawawekea vikwazo wapiganaji wa Colombia nchini Sudan
Kundi la kwanza la waliofukuzwa kutoka Marekani lawasili Kinshasa nchini DRC
Mtoto wa Mugabe akiri kumtishia mtu kwa bunduki nchini Afrika Kusini
Nigeria yapiga marufuku kusimikwa kwa ‘Wafalme wa Igbo’ nje ya nchi
Mawaziri wa mambo ya nje wa Uturuki, Misri, Pakistan, Saudia kukutana Jukwaa la Diplomasia Antalya
Somalia inasema hatua ya Israel kuunga mkono Somaliland inakiuka Uhuru wa Somalia
Mwakilishi Maalumu wa Jumuiya ya Madola Lazarus Chakwera ahitimisha ziara yake nchini Tanzania
Kenya yaomba msaada wa haraka kutoka Benki ya Dunia huku ikipunguza VAT
Wadau wajadili fursa za uwekezaji katika Kongamano la Biashara linaloendelea Kigoma, Tanzania
Mbunge Tanzania ataka sekta binafsi iruhusiwe uzalishaji wa nishati ya umeme
Kampuni ya BP yashtakiwa Kenya kufuatia madai ya uchafuzi mazingira kutokana na uchimbaji mafuta
Mashirika ya ndege ya Nigeria yatishia kusitisha huduma kuanzia Aprili 20 kutokana na bei ya mafuta
Somalia yashtumu uteuzi wa balozi wa Israel katika eneo lililojitenga la Somaliland
Uganda inasema inahitaji zaidi ya Dola bilioni moja kusambaza umeme nchini kote
Afrika Kusini yampa kifungo cha miaka mitano jela Julius Malema kwa kufyatua risasi