| Swahili
UTURUKI
1 dk kusoma
Uturuki na Misri zatia saini makubaliano ya kuweka msingi wa ushirikiano katika sekta ya ulinzi
Makubaliano hayo yanaweka mfumo wa ushirikiano mpya kati ya nchi hizo mbili katika sekta ya ulinzi, amesema Katibu Mkuu wa Viwanda vya Ulinzi, Görgün.
Uturuki na Misri zatia saini makubaliano ya kuweka msingi wa ushirikiano katika sekta ya ulinzi
Katibu wa Viwanda vya Ulinzi wa Uturuki, Haluk Gorgun, alimpokea Waziri wa Ulinzi wa Misri, Ashraf Salem Zaher, jijini Ankara. / / AA

Uturuki na Misri zimetia saini makubaliano ya kuweka msingi wa ushirikiano wa karibu zaidi katika sekta ya viwanda vya ulinzi, huku nchi hizo zikilenga kuendeleza uwezo wa pamoja wa kijeshi na ushirikiano wa baadaye.

Katibu Mkuu wa Viwanda vya Ulinzi wa Uturuki, Haluk Görgün, amesema makubaliano hayo yanaweka mfumo wa ushirikiano mpya kati ya nchi hizo mbili katika sekta ya ulinzi.

Görgün, alimkaribisha Waziri wa Ulinzi wa Misri, Luteni Jenerali Ashraf Salem Zaher, pamoja na ujumbe wake katika mji mkuu Ankara siku ya Jumatatu.

Katika taarifa yake kupitia mtandao wa X, Görgün alisema pande hizo mbili zilijadili fursa za ushirikiano katika sekta ya ulinzi pamoja na masuala mengine kadhaa kwa ajili ya maendeleo ya pamoja ya uwezo wa kijeshi.

“Katika muktadha huu, tumetia saini makubaliano ya kuweka msingi wa ushirikiano wetu katika kipindi kijacho,” alisema.

Görgün aliongeza kuwa kuimarika kwa ushirikiano wa viwanda vya ulinzi kati ya Uturuki na Misri kutachangia usalama wa kikanda na kuimarisha uwezo wa nchi zote mbili.

Pia aliwashukuru Zaher na ujumbe wa Misri kwa mazungumzo aliyoyaelezea kuwa yenye tija.

Mapema siku hiyo, Waziri wa Ulinzi wa Uturuki, Yaşar Güler, alikutana na Zaher, ambaye pia ni Kamanda Mkuu wa Jeshi la Wanajeshi la Misri.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Mashambulizi ya Israel yanatishia usalama wa Syria: Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki
Muswada wa “Uturuki Isiyo na Ugaidi” wafungua hatua muhimu katika kukomesha ugaidi: Erdogan
Mkuu wa mawasiliano wa Uturuki anasema Israel inahujumu juhudi za amani za Gaza
Uturuki inaweka historia kwa kusafirisha treni ya kwanza iliyotengenezwa nchini humo kwenda Afrika
Mkuu wa shirika la ujasusi wa Uturuki akutana na kiongozi wa Hamas kujadili mpango wa amani wa Gaza
Rais wa Uturuki na Mwana Mfalme wa Saudia wajadili usalama wa kikanda na mpango wa amani wa Gaza
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki na Kuwait wajadili yanayojiri katika kanda
Mkuu wa mawasiliano wa Uturuki anasema Israel inahujumu juhudi za kutafuta amani Gaza
Uturuki yalaani mashambulizi ya Israel huko Gaza, ikimtuhumu Netanyahu kwa kuhujumu juhudi za amani
Mpango wa 'Uturuki Isiyo na Ugaidi' kupata msukumo kupitia hatua za bunge: Erdogan
Uturuki na Iraq zasaini makubaliano ya kuongeza matumizi ya bomba la mafuta la Kirkuk-Ceyhan
Uturuki yamkamata gaidi wa FETO aliyekuwa akisakwa kwa jaribio la mwaka 2016 la kumuua Rais Erdogan
Sabiha Gokcen ya Istanbul yaongoza kwa ukuaji wa idadi ya abiria kati ya viwanja vya ndege Ulaya
Uturuki yaimarisha utoaji wa misaada duniani, ikisaidia nchi 85
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Sudan wakutana jijini Ankara
Trump apuuza pingamizi la Netanyahu kuhusu uuzaji wa ndege za kivita za F-35 kwa Uturuki
Erdogan wa Uturuki, Faye wa Senegal wajadili uhusiano, masuala ya dunia
Mwanadiplomasia wa Uturuki Fidan ajadili Kupro, Syria na masuala ya kanda na mkuu wa UN Guterres
Mwanadiplomasia mkuu wa Uturuki Fidan ajadili Cyprus, Syria na masuala ya kikanda na Guterres
Lilikuwa ni jambo la kifahari kuandaa mkutano wa NATO jijini Ankara, asema Erdogan