DR Congo katika mazungumzo ya kuwapokea wahamiaji waliofukuzwa nchini Marekani
Mazungumzo na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo bado hayajaleta makubaliano na maelezo muhimu bado hayajatatuliwa, shirika la habari la Reuters linaripoti.
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo iko kwenye mazungumzo na utawala wa Trump kuhusu kupokea watu waliofukuzwa kutoka Marekani, vyanzo viwili vya serikali mjini Kinshasa vililiambia shirika la habari la Reuters, juhudi ya punde zaidi ya makubaliano kama hayo yaliyofikiwa barani Afrika.
Majadiliano hayo, ambayo pia yameelezwa na vyanzo vitatu vya Umoja wa Mataifa na wanadiplomasia wawili waliopewa taarifa na maafisa wa Marekani, yanasisitiza kuongezeka hatua za Washington za kuwafukuza wahamiaji kwa nchi ya tatu ili kuongeza kasi ya kuwaondoa wahamiaji walioingia au kubaki Marekani bila kibali.
Mipango mara nyingi hujadiliwa kwa usiri , na maelezo machache ya umma juu ya upeo au masharti yao.
Mazungumzo hayo na Congo yanaenda sambamba na juhudi za utawala wa Trump kutekeleza makubaliano ya amani kati ya Congo na Rwanda na makubaliano ya kuhakikisha Marekani inapata madini muhimu ya Congo.
Marekani imetuma watu waliofukuzwa katika nchi za Afrika zikiwemo Ghana, Cameroon, Equatorial Guinea na Eswatini, jambo ambalo limekosolewa na wataalamu wa sheria na makundi ya kutetea haki za binadamu kuhusu msingi wa kisheria wa uhamisho huo na jinsi wanavyotendewa wahamishwaji waliotumwa katika nchi ambazo sio zao asili.
Baadhi ya wahamiaji hao wamelazimika kurudi nyumbani licha ya kupata ulinzi ulioamriwa na mahakama nchini Marekani uliokusudiwa kuzuia hilo kutokea.
Mazungumzo na Congo bado hayajaleta makubaliano na maelezo muhimu bado hayajatatuliwa, duru za Congo zilisema. Bado haijajulikana ni lini safari za kwanza za ndege za kufukuzwa zinaweza kufanyika, ni wahamiaji wangapi wanaweza kuhusika au mataifa yao.
Haijulikani pia ni nini Congo, kama ipo, ingepokea kama malipo ya kukubali kuwapokea.
Chanzo ndani ya Shirika la Kimataifa la Uhamiaji la UN (IOM) kilichoelewa mazungumzo hayo kiliiambia Reuters kuwa mpango huo ungeweza kuhusisha wahamiaji kutoka Amerika Kusini, wakiwemo raia wa Venezuela.
Msemaji wa Idara ya Jimbo alisema Washington "haina maoni kuhusu undani wa mawasiliano yetu ya kidiplomasia na serikali nyingine."
Msemaji wa urais wa Congo hakuweza kujibu mara moja ombi la maoni.