Raila Odinga na simulizi ya kutumia pasipoti ya Tanganyika kuingia Ujerumani
Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya, Raila Odinga./Reuters
Raila Odinga na simulizi ya kutumia pasipoti ya Tanganyika kuingia Ujerumani
Pasipoti hiyo ya muda ilitolewa kwa Raila na vijana wengine wawili, kabla ya Tanganyika kuungana na Zanzibar mwaka 1964 na kuzaliwa Tanzania.
16 Oktoba 2025

Unajua kuwa hati ya kwanza ya kusafiria ya Raila Odinga ilitolewa jijini Dar es Salaam mwaka 1962 katika nchi iliyofahamika kama Tanganyika?

Ni hati hiyo hiyo, iliyotumiwa na Waziri Mkuu huyo wa zamani wa Kenya kuingia Ujerumani Mashariki kwa ajili ya masomo yake ya elimu ya juu.

Pasipoti hiyo ya muda ilitolewa kwa Raila na vijana wengine wawili, kabla ya Tanganyika kuungana na Zanzibar mwaka 1964 na kuzaliwa Tanzania.

Kulingana na Raila mwenyewe, hii ilitokana na kwamba idara ya uhamiaji ya Kenya ambayo ilikuwa chini ya Uingereza kwa wakati huo, kumnyima hati ya muhimu, na badala yake, Waziri Mkuu wa Tanganyika kwa wakati huo, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ambaye alikuwa swahiba wa baba mzazi wa Raila, Jaramogi Oginga Odinga, kumpatia pasipoti hiyo kutoka Tanganyika.

Hii ni kwa mujibu wa simulizi inayopatikana katika kitabu chake cha ‘The Flame of Freedom’ kilichozinduliwa mwaka 2013.

Raila, ambaye alikuwa na umri wa miaka 17, wakati huo akiwa kidato cha pili, alitakiwa aende kusoma nje ya nchi, kutokana na mahusiano mazuri kati ya Jaramogi Odinga na nchi za Umoja wa Kisoveti, tofauti na ilivyokuwa kwa serikali ya Uingereza.

Kwa upande wake, kaka yake mkubwa, Oburu Odinga ambaye alikuwa ameshatangulia kuelekea kwenye umoja wa nchi za Kisovieti, hakunyimwa tu fursa ya kujiunga na shule nzuri za Kenya, bali pia alinyimwa pasipoti ya kumwezesha kwenda nje ya nchi.

“Ombi la Oburu lilikataliwa mapema kabisa, kwa kisingizio kwamba pasipoti ya Jaramogi ilikuwa ikishikiliwa na serikali kwa sababu alikuwa ametembelea nchi za Kisoveiti na China. Kwa wakati huo, Jaramogi alikuwa akitumia pasipoti za kimataifa alizopewa na Kwame Nkrumah na Gamal Abdiel Nasser,” anasema Raila katika kitabu hicho.

Anaongeza: Katika kipindi hicho, Jaramogi alijua kwamba ili tupate elimu nzuri, basi ilitupasa tukasome nje ya nchi.

Kulingana na Raila, mmoja wa wasaidizi wa baba yake aitwaye Okuto Bala, alimchukua kutoka shule ya sekondari Maranda iliyopo Nyanza na kupelekwa Nairobi, kisha Dar es Salaam.

“Kipindi hicho barabara ya lami kutoka jiji la Nairobi iliishia njia panda ya uwanja wa ndege…kutoka hapo mpaka Namanga ilikuwa ni vumbi. “Tulipitia Korogwe, Handeni na kisha Morogoro ambapo lami ilianza tena.”

Kwa mujibu wa Raila, walifika Dar es Salaam saa moja na nusu asubuhi, na saa 24 baadaye, walipokelewa na Dola Osman, aliyekuwa msaidizi binafsi wa Katibu Mkuu wa chama cha TANU, Oscar Kambona.

“Tulikaribishwa vizuri, tukawekwa hotelini na baada ya kuoga na kubadilisha mavazi yetu, Osman alikuja kutupokea na kuchukua picha zetu tatu za pasipoti,” anaeleza Raila.

Baada ya hatua kadhaa za kushughulikia pasipoti zao, Raila na kaka yake walipata fursa ya kutembelea jiji la Dar es Salaam kabla ya kukutana na Mwalimu Nyerere.

“Mwalimu alifurahi sana kutuona, alituambia kuwa alikuwa rafiki mzuri wa Jaramogi…tulipata mlo pamoja na Mwalimu Nyerere, kabla hajatutakia safari njema na masomo mema,” anasema Raila katika kitabu hicho.

Tazama video ya Raila akielezea alivyotumia pasipoti ya Tanganyika

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi
AU yakanusha tuhuma za Trump kuhusu mauaji ya halaiki Nigeria
Mwigulu Nchemba ateuliwa Waziri Mkuu Tanzania
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti