Changamoto za mzazi wa kiume au maarufu "single fatherhood"
Single Fatherhood
Changamoto za mzazi wa kiume au maarufu "single fatherhood"
Baba asiye na mke au mwenza anaweza kuwa na wasiwasi ikiwa anaweza kumtunza mtoto wake vizuri na kunaweza kuwa na maeneo ambapo anahisi upungufu wa kibinafsi na anahitaji msaada kutoka kwa wengine.
18 Julai 2025

Familia zinabadilika kote ulimwenguni na familia za mzazi mmoja zinazidi kuwa za kawaida katika nchi nyingi, hasa kutokana na kuongezeka kwa viwango vya talaka na wanandoa kupata watoto nje ya ndoa.

Mara nyingi utakuta familia hizi huwa za mama pekee, lakini katika miaka ya hivi karibuni, kina baba wengi wamejitolea kulea watoto wao wakiwa peke yao. Kina baba mara nyingi huenziwa kwa furaha na muunganisho wake, lakini kwa kina baba wasio na wenza, jukumu hili linakuwa na changamoto za kipekee ambazo mara nyingi hazichukuliwi kwa uzito.

Katika jamii zetu, hasa za Kiafrika, jamii, familia, na tamaduni zina matarajio tofauti inapokuja kwa majukumu ya kijinsia na kama inafaa kwa mwanamume kuchukua jukumu la mlezi mkuu katika familia. Changamoto hii ni kukabiliwa na unyanyapaa kutoka kwa jamii kwa mtazamo wa jamii au fikra potofu. Mitazamo fulani inaweza kufanya iwe vigumu kwa baba wa watoto kupata usaidizi unaohitajika wakati wa shida.

Baba asiye na mke au mwenza anaweza kuwa na wasiwasi ikiwa anaweza kumtunza mtoto wake vizuri na kunaweza kuwa na maeneo ambapo anahisi upungufu wa kibinafsi na anahitaji msaada kutoka kwa wengine.

Kwa Bashir Idris Abubakar kutoka Nigeria, alijikuta katika hali ya kuwa mzazi pekee baada ya msiba. Alifunga ndoa na mkewe mwisho wa mwaka wa 2020 na kujaaliwa mtoto wa kike mwisho wa mwaka wa 2021. Baada ya miaka miwili, Bashir alipata kazi nje ya nchi na akasafiri na kumuacha mkewe akiwa mjamzito na mtoto wa pili.

Alipokuwa huko, mkewe aliugua na akaaga dunia. Kwa Bashir, hili lilimvunja moyo sana kwani alikuwa ameazimia kujenga maisha yake na mkewe na watoto wao. Changamoto ya kwanza kwake ni kuzowea maisha bila mkewe, jambo ambalo bado anapambana nalo.

Bashir ilibidi amuache mwanawe Nigeria alelewe na familia yake. Ijapokuwa anashukuru kupata usaidizi kutoka kwa familia yake kumsaidia kumlea mwanawe anahisi kuwa yeye kama baba hapati nafasi ya kuwa katika maisha ya mwanawe na kuweza kumlea anavyohisi kuwa ndiyo malezi anayotaka mwanawe awe nayo. Hii ni changamoto inayowakumba kina baba wengi ya kuweka mizanina ya majukumu ya kazi na ulezi.

Soma zaidi
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti
Nigeria yaanzisha uchunguzi baada ya kukamata kilo 1,000 za kokeini yenye thamani ya $235M
Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam
Mtoto wa Gaddafi aachiliwa huru baada ya miaka kumi gerezani
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Zaidi ya mataifa 20 yanalaani ukatili wa RSF nchini Sudan, na kutaka kukomeshwa kwa ghasia
Rais wa Misri, afisa mkuu wa usalama wa Urusi kujadili ushirikiano wa kijeshi
Maelfu ya wananchi wanashikiliwa katika hali mbaya sana katika Al Fasher, Sudan: madaktari
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aghairi ziara iliyopangwa nchini Kenya
‘Mauaji ya waandamanaji ni chukizo mbele za Mungu’
Jeshi la Sudan lazima shambulio la RSF katika mji wa Babnousa huko Kordofan Magharibi
Majeshi ya Somalia yawaua viongozi watatu wakuu wa Al Shabaab
Rwanda, DRC zaanzisha mfumo wa ushirikiano wa kiuchumi huku kukiwa na mazungumzo ya amani
RSF yazika miili katika makaburi ya halaiki, inachoma wengine ili 'kuficha ushahidi wa mauaji
Wananchi katika Al Fasher, Sudan, wanakabiliwa na ukatili 'wa kiwango kisichoweza kuaminika' — UN