| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
UN yaelezea unyanyasaji wa kingono DRC, makundi yenye yatajwa kuhusika
Takriban asilimia 80% ya wale walioathirika wako katika mikoa ya mashariki ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini, data za Umoja wa Mataifa zinaonesha
UN yaelezea unyanyasaji wa kingono DRC, makundi yenye yatajwa kuhusika
DRC
9 Machi 2026

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (MONUSCO) siku ya Jumatatu imeonya kuhusu kuzidi kwa unyanyasaji wa kingono katika nchi hiyo yenye mgogoro, ukieleza kuwa makundi yenye silaha yanahusika kwa matukio mengi yaliyoorodheshwa 2025.

Ofisi ya Umoja ya Mataifa kuhusu Haki za Binadamu (UNJHRO) imeorodhesha matukio 887 yaliyohusisha waathiriwa 1,534, ikiwemo wanawake 854 na wasichana 672, kulingana na taarifa kutoka MONUSCO.

Mikoa ya mashariki ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini ndiyo yenye matukio mengi zaidi ikiwa na asilimia 80% ya waathiriwa, ilisema.

UNJHRO imebaini kuwa makundi yenye silaha yanahusika na kwa asilimia 75% ya waathiriwa, huku kundi la waasi la M23 likihusika na idadi kubwa ya matukio (439), likifuata na wapiganaji wa Wazalendo, CODECO, makundi mbalimbali ya Mai-Mai, FDLR, na ADF.

Pia ilieleza wasiwawasi kuhusu baadhi ya maafisa wa serikali, ikisema wanajeshi, polisi, na idara ya ujasusi imehusika karibu katika tukio moja kati ya matano ya unyanyasaji wa kingono.

UNJHRO imeonya kuwa ubakaji ulikuwa unatumiwa kama vita nchini Congo, huku wanawake na wasichana wakifanywa watumwa wa kingono na kizazi kingine cha watoto kikikumbwa na unyanyapaa na kutengwa.

Pia inaeleza kuhusu madhila ya watoto waliozaliwa kutokana na ubakaji, ambao hukataliwa na familia, kutosajiliwa, na wanakuwa katika hatari kubwa ya kutengwa kijamii na mara moja huchukuliwa na makundi yenye silaha.

MONUSCO inasema mbali na kuwa asilimia 70% ya walionusurika wanapata huduma za dharura za afya, ni chini ya asilimi 2% wanaopata usaidizi kamili, ikiwemo msaada wa kisheria, kisaikolojia, na wa kijamii.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Watu kumi na nne waliotekwa Nigeria waokolewa: Gavana wa Jimbo
Ziara ya Afrika: Papa Leo afanya Misa nchini Angola
Wamefukuzwa Sahel: Ufaransa inatafuta nini nchini Kenya?
Pande zinazopigana DR Congo zimekubaliana kubadilishana wafungwa na kuruhusu ufikiaji wa msaada
Nigeria yavamia ‘kiwanda cha watoto’ huko Lagos, na kuwaokoa wanawake wajawazito
Marekani yawawekea vikwazo wapiganaji wa Colombia nchini Sudan
Kundi la kwanza la waliofukuzwa kutoka Marekani lawasili Kinshasa nchini DRC
Mtoto wa Mugabe akiri kumtishia mtu kwa bunduki nchini Afrika Kusini
Nigeria yapiga marufuku kusimikwa kwa ‘Wafalme wa Igbo’ nje ya nchi
Mawaziri wa mambo ya nje wa Uturuki, Misri, Pakistan, Saudia kukutana Jukwaa la Diplomasia Antalya
Somalia inasema hatua ya Israel kuunga mkono Somaliland inakiuka Uhuru wa Somalia
Mwakilishi Maalumu wa Jumuiya ya Madola Lazarus Chakwera ahitimisha ziara yake nchini Tanzania
Kenya yaomba msaada wa haraka kutoka Benki ya Dunia huku ikipunguza VAT
Wadau wajadili fursa za uwekezaji katika Kongamano la Biashara linaloendelea Kigoma, Tanzania
Mbunge Tanzania ataka sekta binafsi iruhusiwe uzalishaji wa nishati ya umeme
Kampuni ya BP yashtakiwa Kenya kufuatia madai ya uchafuzi mazingira kutokana na uchimbaji mafuta
Mashirika ya ndege ya Nigeria yatishia kusitisha huduma kuanzia Aprili 20 kutokana na bei ya mafuta
Somalia yashtumu uteuzi wa balozi wa Israel katika eneo lililojitenga la Somaliland
Uganda inasema inahitaji zaidi ya Dola bilioni moja kusambaza umeme nchini kote
Afrika Kusini yampa kifungo cha miaka mitano jela Julius Malema kwa kufyatua risasi