Tetemeko la ardhi la kiwango cha 7.4 laua mtu mmoja Indonesia na kusababisha tahadhari za tsunami

Tetemeko la ardhi la kiwango cha 7.4 katika Bahari ya Molucca, na kusababisha tahadhari za tsunami katika eneo hilo pamoja, maafisa waendelea kuthibitisha idadi ya vifo na kutathmini uharibifu wa miundombinu.

By
Mwanamume aonekana akikagua vifusi kwenye eneo la jengo lililoharibiwa kufuatia tetemeko la ardhi huko Manado. / / Reuters

Tetemeko hilo lilitokea mapema alfajiri ya Alhamisi katika sehemu ya kaskazini ya Bahari ya Molucca mashariki mwa Indonesia, likiua angalau mtu mmoja na kusababisha tahadhari za tsunami katika baadhi ya maeneo ya ukanda huo.

Kifo hicho kiliripotiwa katika mji wa Manado, kwa mujibu wa Antara News.

Kituo cha televisheni cha Metro TV kilisema mwathiriwa alifariki baada ya kuangukiwa na vifusi, picha zilionyesha majengo yaliyoharibika katika eneo hilo.

Mfumo wa kutoa tahadhari ya Tsunami ya Marekani ulitoa taarifa ya kwamba mawimbi yanaweza kutokea ndani ya umbali wa kilomita 1,000 kutoka kitovu cha tetemeko, na yanaweza kuathiri pwani za Indonesia, Ufilipino na Malaysia.

Tetemeko hilo lilitokea katika kina cha kilomita 35, na kitovu chake kikiwa takribani kilomita 127 magharibi-kaskazini magharibi mwa Ternate, kulingana na Utafiti wa Jiolojia wa Marekani. Mji huo una wakazi zaidi ya 205,000.

Operesheni za uokoaji zinaendelea

Abdul Muhari, mkuu wa Shirika la Kitaifa la Usimamizi wa Maafa nchini Indonesia, alisema maafisa walioko Manado na Bitung katika eneo la Kaskazini mwa Sulawesi, pamoja na Ternate katika Maluku Kaskazini, waendelea na ukaguzi wa majengo na kutafuta waathirika wengine.

“Bado tunakusanya taarifa kuthibitisha idadi ya waathirika na kiwango cha uharibifu katika kila eneo,” Muhari aliambia ABC News ya Australia.

Mamlaka katika maeneo kadhaa, ikiwa ni pamoja na Ternate na Tidore — ambazo ni sehemu ya visiwa vya kihistoria vya Spice Islands — waliwahimiza wakazi kujiandaa kwa uwezekano wa kuhama.

Indonesia iko katika ukanda wa ‘Pacific Ring of Fire’, eneo lenye shughuli nyingi za kijiolojia ambapo mabamba ya ardhi hukutana, na kusababisha matetemeko ya ardhi na shughuli za volkano mara kwa mara.