| Swahili
ULIMWENGU
2 dk kusoma
Ndege mpya ya Trump haina baadhi ya mifumo ya kujihami: Ripoti
Jeshi la Anga la Marekani limekiri kuwa ndege hiyo haina vifaa vyote vinavyohitajika kwenye Air Force One.
Ndege mpya ya Trump haina baadhi ya mifumo ya kujihami: Ripoti
Wataalamu wanaonya kuwa Boeing 747-8 aliyozawadiwa na Qatar inaweza kuongeza kiwango cha hatari katika safari za kimataifa. /

Ndege mpya ya Air Force One aliyotumia Rais Donald Trump kusafiria Uturuki haina baadhi ya mifumo ya kujihami iliyokuwepo kwenye ndege ya awali ya rais, ikiwemo uwezo wa hali ya juu wa kujikinga dhidi ya makombora, kwa mujibu wa ripoti ya gazeti la The New York Times iliyowanukuu maafisa wa Marekani.

Wataalamu wanaonya kuwa Boeing 747-8 aliyozawadiwa na Qatar inaweza kuongeza kiwango cha hatari katika safari za kimataifa, huku ripoti zikidai kuwa Walinzi Rasmi wa Viongozi Marekani walimshauri Trump kurudi Marekani kwa kutumia Air Force One ya zamani.

Ikulu ya White House ilitetea usalama wa ndege hiyo, lakini haikutoa maelezo kuhusu uwezo mahsusi. Msemaji wa Ikulu, Steven Cheung, alisema: "Air Force One mpya ni ndege ya kisasa yenye viwango vya juu vya usalama ambayo imewekewa mifumo madhubuti ya kulinda usalama wa rais na wafanyakazi wake."

Jeshi la Anga la Marekani limekiri kuwa ndege hiyo haina vifaa vyote vinavyohitajika kwenye Air Force One . Limeieleza kuwa ni ndege ya muda itakayotumika hadi ndege mbili mpya za rais zinazotengenezwa na Boeing zitakapokamilika.

Katika taarifa ya Juni 19, Jeshi la Anga lilisema: "Wamechukua tahadhari zote za kiusalama, ulinzi na mawasiliano ya misheni."

Hata hivyo, maafisa wanaofahamu mchakato wa maboresho ya ndege hiyo walisema haijapewa mifumo sawa ya kujihami dhidi ya mashambulizi kama ilivyokuwa kwa ndege ya awali, ingawa Jeshi la Anga halijabainisha ni mifumo gani hasa iliyoachwa.

Maafisa wawili wa zamani wa Jeshi la Anga waliokuwa sehemu ya mpango wa kubadilisha ndege ya rais walisema walishangazwa na uamuzi wa Trump kuitumia ndege hiyo katika safari ya nje ya nchi, wakieleza kuwa mazingira ya usalama katika safari hizo huwa na hatari kubwa zaidi.

Waliongeza kuwa kasi ya maandalizi huenda haikuruhusu muda wa kutosha wa kufunga mifumo yote ya usalama ambayo kwa kawaida hupatikana kwenye Air Force One iliyokamilika.

 

 

CHANZO:AA
Soma zaidi
Iran yatishia kushambulia mitambo ya umeme ya nchi za Ghuba iwapo Marekani itashambulia mitambo yake
Nchi 20 za Kiislamu zajadili hatua za pamoja dhidi ya ukiukaji wa Israel katika Msikiti wa Al-Aqsa
Mawaziri wa bara Arabu, Waislamu wakutana Jordan kujadili kwa pamoja Jerusalem Mashariki inayokaliwa
Wahamiaji 70,000 waondoka Hispania huku idadi ya vifo ikiongezeka
Wanafunzi wa Korea Kusini matatani kwa ‘kuvunja’ na kuingia ndani ya kambi ya kijeshi ya Marekani
Wahamiaji wapatao 160 waokolewa baada ya meli yao kuwaka moto
Chama cha soka cha Palestina chaituhumu FIFA kwa kushindwa kuiadhibu Israel
Trump aitaka Iran ichague kati ya makubaliano na kujislamisha
Namna kijana mwenye umri wa miaka 12 mwenye usonji alivyotumia uokaji keki kukabiliana na chuki
Australia yathibitisha vifo vya ndege vinavyotokana na mafua H5
Iran: Hatuna mazungumzo yoyote na Marekani
Mashambulizi ya Israel yaua Wapalestina 12, wakiwemo watoto wawili, huko Gaza
Iran inachukulia kila tishio kutoka kwa wapinzani kuwa "halisi na la kuaminika" : Kaimu Waziri
Trump asitisha shambulio lililopangwa dhidi ya Iran
Hamas yakubali kusalimisha silaha nzito katika 'uamuzi mgumu' kama sehemu ya makubaliano
Makubaliano ya nyuklia ya Marekani na Saudi Arabia yanabadilisha muelekeo Mashariki ya Kati
Taifa la Nauru labadilisha jina, sasa kuitwa Naoero
China yakana taarifa za kusafirisha vifaa vya kurusha makombora Iran
Marekani yaanzisha wimbi jipya la mashambulizi dhidi ya Iran
Watu wasiojulikana waharibu kituo cha hija ya Wakatoliki nchini Bosnia