| Swahili
ULIMWENGU
2 dk kusoma
Marekani kuwaondoa wanajeshi 5,000 kutoka Ujerumani katikati ya mtafaruku kutokana na vita vya Iran
Pentagon inasema uondoaji wa wanajeshi wa Marekani unatarajiwa kukamilika katika kipindi cha miezi sita hadi kumi na miwili ijayo.
Marekani kuwaondoa wanajeshi 5,000 kutoka Ujerumani katikati ya mtafaruku kutokana na vita vya Iran
Ujerumani ndilo eneo kubwa zaidi la kijeshi la Marekani barani Ulaya, likiwa na wanajeshi 35,000 wanaofanya kazi. [Faili] / Reuters / Reuters

Waziri wa Ulinzi wa Marekani Pete Hegseth ameamuru kuondolewa kwa wanajeshi 5,000 kutoka Ujerumani ndani ya mwaka ujao, Pentagon ilisema.

Tangazo la Ijumaa lilikuja baada ya Rais Donald Trump kusema mapema wiki hii kwamba ataondoa wanajeshi kutoka mshirika wa NATO Ujerumani huku kukiwa na mzozo na Kansela wake, Friedrich Merz, kuhusu vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran.

"Tunatarajia uondoaji huo utakamilika katika kipindi cha miezi sita hadi kumi na miwili ijayo," msemaji wa Pentagon Sean Parnell alisema katika taarifa.

"Uamuzi huu unafuatia mapitio ya kina ya uwepo wa nguvu wa Idara huko Ulaya na ni kwa kutambua mahitaji ya oparesheni na masharti ya msingi," Parnell aliongeza.

Trump alisema Jumanne kwamba Merz "anafikiri ni sawa kwa Iran kuwa na Silaha ya Nyuklia. Hajui anachozungumzia!"

Siku ya Jumatano, Trump alisema Washington ilikuwa "inasoma na kukagua uwezekano wa kupunguzwa" kwa wanajeshi wa Marekani nchini Ujerumani, na kwamba angeamua "katika muda mfupi."

'Kwanini nisifanye hivyo?'

Siku ya Alhamisi, Trump alisema anaweza kuwaondoa wanajeshi wa Marekani kutoka Italia na Uhispania kutokana na kukosa uungwaji mkono wakati wa vita, akiwaambia waandishi wa habari katika Ofisi ya Oval: "Italia haijatusaidia chochote na Uhispania imekuwa ya kutisha, ya kutisha kabisa."

"Ndiyo, pengine, pengine nitaondoa. Nini kinanizuia kufanya hivyo ?" Trump alisema.

Kufikia Desemba 31, 2025, kulikuwa na wanajeshi 12,662 wa Marekani waliokuwa kazini nchini Italia na 3,814 nchini Uhispania. Ujerumani walikuwa 36,436.

Akizungumza katika ziara yake nchini Morocco, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani Johann Wadephul alisema Alhamisi kwamba Ujerumani "imejiandaa" kwa ajili ya kupunguzwa kwa wanajeshi wa Marekani na "anaijadili kwa karibu na kwa moyo wa kuamini mashirika yote ya NATO."

Huku akisema "ameridhika" kuhusu wazo la kuwa na wanajeshi wachache wa Marekani nchini Ujerumani, Wadephul alisema kuwa kambi kubwa za Wamarekani nchini Ujerumani "hazijajadiliwa hata kidogo."

Alisema kwa mfano kwamba Uwanja wa Ndege wa Ramstein ulikuwa na 'kazi isiyoweza kubadilishwa kwa Marekani na kwetu pia.'

EU ilisema Alhamisi kwamba uwekaji wa wanajeshi wa Marekani barani Ulaya ulikuwa katika maslahi ya Washington, na kwamba Marekani ilikuwa 'mshirika wa muhimu katika kuchangia usalama na ulinzi wa Ulaya.'

CHANZO:TRT World and Agencies