Uturuki inakabiliwa na "janga" wakati kiwango cha uzazi kinashuka hadi 1.48, anaonya Erdogan

Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, amesema kwamba kupungua kwa kiwango cha uzazi kunatoa onyo kali za tahadhari kuhusu mustakabali wa nchi, na kwamba hakuna anayeuthamini mustakbali wa taifa hili anayeweza kukaa kimya.

By
Uturuki inakabiliwa na "janga" wakati kiwango cha uzazi kinapungua. / / AA

Akihutubia Kongamano la Familia na Utamaduni-Sanaa Alhamisi jijini Ankara, Erdogan alisisitiza changamoto zinazozidi kukua zinazoikabili taasisi ya familia.

Akiangazia changamoto kwa taasisi ya familia, Erdogan alisema, "Tunachukua hatua dhidi ya matakwa ya kutoegemea upande wa kijinsia na mienendo ya LGBT, bila ya kulegeza kamba."

Alisisitiza kwamba Uturuki inalinda taasisi ya familia katika kipindi ambacho ubepari wa kimataifa unafungua uwanja mpya wa mapambano, huku ubeberu wa kitamaduni na udhibiti wa kidijitali vikiongezeka duniani kote.

Rais huyo pia alionya kuhusu mzozo wa idadi ya watu, akisema: “Kwa sasa tunakabiliwa na janga,” baada ya takwimu rasmi kuonyesha kuwa kiwango cha jumla cha uzazi nchini kimeshuka hadi 1.48 mwaka jana.

Erdogan alisema kushuka kwa kiwango cha uzazi “ni onyo kali sana za hatari kwa mustakabali wetu,” na kwamba “hakuna anayeuthamini mustakabali wa nchi hii anayeweza kuwa kukaa kimya au kutojali.”

Mwezi Mei, Erdogan alitangaza kwamba Uturuki itazingatia miaka ya 2026 hadi 2035 kuwa “Muongo wa Familia na Idadi ya Watu” wakati wa hotuba yake katika Jukwaa la Kimataifa la Familia lililofanyika Istanbul.

Erdogan alikosoa mtindo wa kisasa wa maisha unaoweka mbele starehe ya mtu binafsi kuliko uhusiano wa kifamilia na kijamii, akisema:

“Mtazamo wa kisasa unaojengwa kwa dhana za kuishi bila familia na upweke hauwezi kuleta amani kwa mtu binafsi wala kwa jamii.”

“Mtindo huu wa maisha unaingia kwa kasi katika misingi ya jamii yetu, kuanzia kwa vijana,” alisema.

Nchi nyingi nyingine pia zimechukua hatua dhidi ya harakati za LGBT.

Urusi ilipiga marufuku ‘harakati ya kimataifa ya LGBT’ mwaka 2023.

Hivi karibuni, Hungary, Bulgaria, Argentina, Indonesia na Georgia zimepitisha hatua zinazolenga kulinda maadili ya kifamilia dhidi ya ushawishi wa LGBT.

Vilevile, zaidi ya nchi 30 za Afrika, nchi 22 za Asia, mataifa sita ya Marekani na sita katika Oceania zimepitisha hatua kali dhidi ya mashinikizo ya ujinsia usioegemea upande wowote.