| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Maambukizi ya Ebola DRC yaongezeka hadi 282, serikali imesema
Maambukizi yaliyothibitishwa ya Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo sasa yamefikia 282, serikali ya taifa hilo la Afrika ya Kati ilisema siku ya Jumapili.
Maambukizi ya Ebola DRC yaongezeka hadi 282, serikali imesema
Idadi ya maambukizi ya Ebola DRC imeongezeka hadi 282, serikali imesema Juni 1, 2026. / Reuters

Kuna maambukizi yasiyopungua 282 ya Ebola yameripotiwa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, taifa hilo la Afrika ya kati lilisema siku ya Jumapili, huku wagonjwa waliopona wakieleza furaha yao katika mahojiano na shirika la Associated Press.

Mlipuko huo bado uko zaidi katika mkoa wa mashariki mwa DRC wa Ituri, ambapo kuna maambukizi 264 yameripotiwa, Wizara ya Afya ya DRC imesema.

Katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kumekuwa na ripoti za maambukizi zaidi ya 1,000 ya aina ya virusi vya Bundibugyo, ambavyo havina tiba au chanjo iliyothibitishwa kwa sasa.

Furaha ya wagonjwa waliopona

Kutafuta watu waliotangama kumesaidia kuwafikia asilimia 45 huku 220 wanaoshukiwa wakiwa chini ya uangalizi, wizara imesema.

Wakati huohuo, baadhi ya watu watano waliopona ugonjwa huo walizungumza kuhusu ahuweni waliopata katika mahojiano na Associated Press.

Baraka Bulambulu, muuguzi, anasema alikuwa na furaha sana baada ya vipimo viwili vya Ebola kuonesha kuwa hana tena ugonjwa huo.

Bulambulu ilikuwa sehemu ambayo wale waliopona walipewa vyeti na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani Tedros Adhanom Ghebreyesus wakati akifungua kituo kipya cha kutibu Ebola huko Bunia, mji mkuu wa mkoa wa Ituri, siku ya Jumapili.

Ujasiri unaotoa 'matumaini'

Kwa sasa tiba imelenga dalili zinazoonekana kwa wagonjwa.

Nchi jirani ya Uganda pia kumeripotiwa maambukizi tisa ya Ebola na kufunga mpaka wake na DRC kwa lengo la kupunguza kuenea kwa maambukizi.

Pamoja na kuwepo zaidi ya milipuko 20 ya Ebola nchini DRC na Uganda, aina hii ya virusi vya Bundibugyo ni tofauti. Kutokuwepo kwa chanjo na tiba ilioidhinishwa, pamoja na maeneo ya mbali na mapigano, kumefanya kukabiliana na hali hii kuwa vigumu.

'Kusherehekea ushindi'

Licha ya changamoto hizi, kwa wale waliopona ni muhimu “kusherehekea ushindi,” amesema Dkt. Dieudonne Mwamba Kazadi, mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Afya ya Umma ya DRC.

"Ni ujumbe muhimu kuwa inawezekana mtu kupona Ebola pale anapopata matibabu mapema katika kituo cha afya kilichoidhinishwa,” aliongeza.

CHANZO:TRT Afrika Swahili