| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Watu 280,000 wakosa makazi kufuatia mapigano ya Sudan Kusini: Umoja wa Mataifa
Katika jimbo kuu la Bor, madaktari katika hospitali ya mji wanapambana kutibu ongezeko la watu waliokosa makazi wakati huo huo huduma za msingi zikikosekana.
Watu 280,000 wakosa makazi kufuatia mapigano ya Sudan Kusini: Umoja wa Mataifa
Mashirika ya kutoa misaada ya kibinadamu yanasema hali inaendelea kuwa mbaya. / Others
6 Machi 2026

Mapigano mapya katika jimbo la Jonglei kati ya vikosi vitiifu kwa Rais Salva Kiir na wapiganaji wanaohusishwa na aliyekuwa Makamu wa Rais Riek Machar yamefanya takriban watu 280,000 kukosa makazi tangu Disemba, kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.

Sudan Kusini imepata uhuru kutoka Sudan mwaka 2011 lakini muda mfupi baadae ikaingia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya Kiir na Machar, waliokuwa washirika ambao uhasama wao umeigawa nchi katika misingi ya kisiasa na kikabila.

Maafisa wa misaada ya kibinadamu wanasema watu wapatao 825,000 katika jimbo la Jonglei, jimbo la Unity, na jimbo la Eastern Equatoria wanakabiliwa na tatizo la utapia mlo baada ya upungufu wa chakula na kusitishwa kwa huduma muhimu.

Katika jimbo kuu la Bor, madaktari katika hospitali ya mji wanapambana kutibu ongezeko la watu waliokosa makazi wakati huo huo huduma za msingi zikikosekana.

Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali David Tor amesema kituo hicho hakina uwezo wa kudumu ongezeko la wagonjwa.