Burkina Faso yafuta vyama vyote vya kisiasa kwa madai ya Kusababisha 'mgawanyiko'
Waziri wa Utawala Emile Zerbo alisema upigaji marufuku wa vyama hivyo ni baada ya mamlaka kubaini kuwa vyama vimekiuka miongozo iliyowaanzisha.
Serikali ya Burkina Faso imefuta vyama vyote vya siasa nchini na kuondoa sheria zote zinazosimamia vyama hivyo, kwa mujibu wa amri iliyothibitishwa na serikali.
Shughuli za vyama vya siasa zimekuwa zilikuwa zimesimamishwa kwa muda mrefu nchini humo chini ya utawala wa Traore. Amri mpya inavitaka vyama vya kisiasa kuhamisha umiliki wa mali zao kwa serikali, imesema taarifa ya Shirika la Habari la serikali.
Waziri wa Utawala Emile Zerbo alisema upigaji marufuku wa vyama hivyo ni baada ya mamlaka kubaini kuwa vyama vimekiuka miongozo iliyowaanzisha.
Serikali inaamini kwamba kuongezeka kwa idadi ya vyama vya siasa kumesababisha mwenendo wa kupita mipaka, kusababisha mgawanyiko miongoni mwa wananchi na kudhoofisha mshikamano wa kijamii, alisema baada ya kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika Alhamisi, ambapo hatua hiyo ilipitishwa.
Rasimu za sheria zitakazotoa mwongozo kwa kuanzishwa kwa vyama na makundi ya kisiasa zitawasilishwa bungeni 'haraka iwezekanavyo,' alisema waziri.
Tangu walipochukua madaraka katika mapinduzi ya kijeshi mwaka 2022, serikali imeanzisha mabadiliko makubwa, yakiwemo kuchelewesha uchaguzi uliotarajiwa kurejesha utawala wa kiraia na kuiondoa tume huru ya uchaguzi ya nchi.