Chombo cha Uturuki cha baharini, Marlin, kimefanikisha uwezo wake wa kutegesha mabomu, kikitegemea mabomu ya baharini ya Malaman.
Marlin kilikuwa chombo cha kwanza kisichokuwa na nahodha (USV) cha Jeshi la Wanamaji la Uturuki. Kilitengenezwa kwa ushirikiano kati ya kampuni ya Sefine na shirika la jeshi la Aselsan chini ya uratibu wa Shirika la Uturuki la Vifaa vya Kijeshi (SSB).
Kuunganisha huku kwa mabomu ya baharini ya Malaman yaliyotengenezwa Uturuki kwenye Marlin kumedhihirisha hatua muhimu katika uwezo wa kutega mabomu baharini. Mabomu hayo yalitengenezwa na kampuni ya Sefine,kituo cha utafiti SISAM na KocDefense.
Mwaka mmoja wa juhudi za pamoja umezaa matunda ya uwezo wa kutega mabomu kwa kutumia mfumo huo unaokwenda sanjari na mahitaji ya operesheni ya Jeshi la Wanamaji la Uturuki.
Uhakiki, majaribio yamekamilika
Hatua ya muundo na uzalishaji wa kutega mabomu ilikamilika, huku mifumo ya kufuatilia mipango ya kuweka mabomu baharini yakijumuishwa kwenye mfumo huo.
Kampuni ya Sefine Shipyard ilikamilisha uhakiki na majaribio ya mifumo hii, wakati ambao Marlin USV ilifanikisha shughuli ya kuweka mabomu baharini kama ilivyopangwa.
Kukamilisha hili kumeimarisha nafasi ya Uturuki kama moja ya nchi chache ambazo zinaweza kutegesha mabomu baharini kwa kutumia USV.
Muundo wa Marlin na kazi zake uliimarishwa, kuongeza kasi, kupunguza hatari, na kuipa uwezo zaidi kwa operesheni za baharini, ambayo inatarajiwa kulipa nguvu zaidi Jeshi la Wanamaji la Uturuki.





















