Rais Donald Trump wa Marekani amemuelezea Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki kama “kiongozi bora”, akiuita mkutano wa NATO kuwa mafanikio makubwa.
“Tumehitimisha kwa mafanikio makubwa mkutano wa NATO hapa nchini Uturuki,” alisema Trump, katika mkutano na wanahabari jijini Ankara.
Kwa upande mwingine, Trump alimshukuru Rais Erdogan kwa kuandaa mkutano huo.
"Ningependa kumshukuru Rais Erdogan, kwa uongozi wake bora. Ni rafiki yangu kwa muda mrefu sasa. Ni mtu shupavu na hodari mwenye kuongoza taifa zuri," aliongeza.
ZILIZOPENDEKEZWA
Kulingana na Trump, viongozi waliohudhuria mkutano huo walijadiliana namna ya kutumia asilimia 5 ya mapato yao ya taifa kwa ajili ya masuala ya ulinzi.
“Kulikuwa na utulivu na umoja mkubwa wakati mkutano wote,” alisema Trump.
CHANZO:AA













