| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Mawaziri wa Ulinzi wa Uturuki na Misri wakutana Ankara kuimarisha ushirikiano wa kiusalama
Uturuki na Misri zinaendelea kuimarisha ushirikiano katika masuala ya usalama, diplomasia na misaada ya kibinadamu baada ya kurejesha uhusiano wao kufuatia miaka kadhaa ya mvutano wa kisiasa.
Mawaziri wa Ulinzi wa Uturuki na Misri wakutana Ankara kuimarisha ushirikiano wa kiusalama
Waziri wa Ulinzi wa Uturuki, Yasar Guler, alimpokea mwenzake wa Misri, Luteni Jenerali Ashraf Salim Zahir, katika hafla rasmi jjini Ankara. / / Türkiye's Ministry of Defence

Uturuki na Misri zinaimarisha ushirikiano wa kijeshi na kikanda huku viongozi wakuu wa ulinzi wa nchi hizo wakikutana jijini Ankara, hatua inayoashiria kuimarika kwa mahusiano baada ya karibu muongo mmoja wa tofauti za kidiplomasia.

Waziri wa Ulinzi wa Taifa wa Uturuki, Yasar Guler, Jumatatu alimkaribisha Mkuu wa Majeshi ya Misri na Waziri wa Ulinzi na Uzalishaji wa Kijeshi, Luteni Jenerali Ashraf Salim Zahir, kwa hafla rasmi ya kijeshi iliyofanyika katika Makao Makuu ya Wizara ya Ulinzi jijini Ankara.

Baada ya nyimbo za taifa na ukaguzi wa gwaride la heshima, viongozi hao walifanya mazungumzo ya faragha yaliyojikita katika kuimarisha uhusiano wa kijeshi kati ya nchi hizo mbili pamoja na kujadili maendeleo ya usalama katika ukanda.

Kutoka mvutano wa kidiplomasia hadi ushirikiano wa kimkakati

Mkutano huo umefanyika wakati Uturuki na Misri zikiendelea na juhudi za kurejesha kikamilifu mahusiano yao baada ya miaka ya ushirikiano finyu, huku sasa zikilenga kushirikiana zaidi katika kukabiliana na changamoto za pamoja za kikanda.

Katika miaka ya hivi karibuni, uhusiano wa nchi hizo umeimarika kwa kasi kupitia kuongezeka kwa ushirikiano wa kisiasa, kiuchumi na kiusalama.

Wakati wa ziara yake rasmi nchini Misri mwezi Februari, Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan alisema nchi yake inalenga kuimarisha ushirikiano na Misri katika biashara ya baharini, usafirishaji, uhuru wa usafiri wa majini na usalama wa baharini.

Erdogan pia alisisitiza kuwa mahusiano ya kiuchumi na utalii yanaendelea kukua, akibainisha kuwa ongezeko la idadi ya watalii linaonyesha mafanikio ya uhusiano huo na kueleza matumaini ya kupanua ushirikiano zaidi katika sekta ya utalii.

Ushirikiano katika kushughulikia migogoro ya kikanda

Mbali na kuimarisha uhusiano wa mataifa mawili, Uturuki na Misri zimekuwa zikiratibu juhudi katika kushughulikia migogoro mbalimbali ya kikanda, ikiwemo juhudi za kutafuta suluhu za kidiplomasia na kukabiliana na changamoto za kibinadamu.

Katika mzozo wa hivi karibuni unaohusisha Iran, Uturuki, Saudi Arabia na Pakistan zilishirikiana na Misri katika juhudi za kutafuta suluhisho ya kidiplomasia na kupunguza mvutano uliokuwa ukiongezeka.

Nchi hizo mbili pia zimeendelea kuratibu juhudi za misaada ya kibinadamu kwa Ukanda wa Gaza, zikisisitiza umuhimu wa kuongeza upatikanaji wa misaada na kutumia njia za kidiplomasia kushughulikia mzozo unaoendelea.

Maafisa wa nchi hizo wanaamini kuwa kuimarika kwa ushirikiano kati ya Uturuki na Misri kutachangia utulivu wa kikanda wakati ambapo Mashariki ya Kati inakabiliwa na changamoto nyingi za kiusalama.

 

CHANZO:TRT World
Soma zaidi
Ukimshambulia mmoja wetu umetushambulia sote, Uturuki, Saudi Arabia na Pakistan wasema
Erdogan kufanya ziara Saudi Arabia atakutana na MBS na Waziri Mkuu wa Pakistan
Mashambulizi ya Israel yanatishia usalama wa Syria: Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki
Muswada wa “Uturuki Isiyo na Ugaidi” wafungua hatua muhimu katika kukomesha ugaidi: Erdogan
Mkuu wa mawasiliano wa Uturuki anasema Israel inahujumu juhudi za amani za Gaza
Uturuki inaweka historia kwa kusafirisha treni ya kwanza iliyotengenezwa nchini humo kwenda Afrika
Mkuu wa shirika la ujasusi wa Uturuki akutana na kiongozi wa Hamas kujadili mpango wa amani wa Gaza
Rais wa Uturuki na Mwana Mfalme wa Saudia wajadili usalama wa kikanda na mpango wa amani wa Gaza
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki na Kuwait wajadili yanayojiri katika kanda
Mkuu wa mawasiliano wa Uturuki anasema Israel inahujumu juhudi za kutafuta amani Gaza
Uturuki yalaani mashambulizi ya Israel huko Gaza, ikimtuhumu Netanyahu kwa kuhujumu juhudi za amani
Mpango wa 'Uturuki Isiyo na Ugaidi' kupata msukumo kupitia hatua za bunge: Erdogan
Uturuki na Iraq zasaini makubaliano ya kuongeza matumizi ya bomba la mafuta la Kirkuk-Ceyhan
Uturuki yamkamata gaidi wa FETO aliyekuwa akisakwa kwa jaribio la mwaka 2016 la kumuua Rais Erdogan
Sabiha Gokcen ya Istanbul yaongoza kwa ukuaji wa idadi ya abiria kati ya viwanja vya ndege Ulaya
Uturuki yaimarisha utoaji wa misaada duniani, ikisaidia nchi 85
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Sudan wakutana jijini Ankara
Trump apuuza pingamizi la Netanyahu kuhusu uuzaji wa ndege za kivita za F-35 kwa Uturuki
Erdogan wa Uturuki, Faye wa Senegal wajadili uhusiano, masuala ya dunia
Mwanadiplomasia wa Uturuki Fidan ajadili Kupro, Syria na masuala ya kanda na mkuu wa UN Guterres