| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Erdogan: Kwa Israel kutambua Somaliland hakutamfaidi yeyote
Nchi katika kanda lazima zitafute suluhu wenyewe kwa matatizo yanayokumba kanda, Erdogan amesema wakati wa mkutano wa pamoja na waandishi wa habari akiwa na Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy jijini Addis Ababa.
Erdogan: Kwa Israel kutambua Somaliland hakutamfaidi yeyote
Rais Recep Tayyip Erdogan na Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed katika mkutano wa pamoja na waandishi wa habari Addis Ababa Februari 17, 2026. / AA
tokea masaa 5

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan siku ya Jumanne alizungumzia kuhusu uamuzi wa israel kuitambua Somaliland kama taifa huru na ikiwa nchi pekee iliyofanya hivyo, akisisitiza kuwa uamuzi huo hautofaidi Somalia wala kanda hiyo.

"Ningependa kusisitiza kuwa kwa Israel kutambua Somaliland hakutafaidi Somaliland wala Pembe ya Afrika," Erdogan amesema katika mkutano wa pamoja na waandishi wa habari akiwa na Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed jijini Addis Ababa.

Uturuki inaamini kuwa nchi katika kanda hii zinatakiwa kutafuta suluhu ya matatizo ya katika kanda yao wenyewe, amesema Erdogan, akitoa wito kwa Pembe ya Afrika kutogeuzwa "kuwa sehemu ya malumbano ya mataifa ya nje.”

Akisisitiza kuhusu ushirikiano kati ya Uturuki na Ethiopia, Erdogan amesema kuwa ni "fahari kubwa" kuwa makampuni zaidi ya 200 ya Uturuki, yenye uwekezaji wa dola bilioni $2.5, yanasaidia kutoa ajira kwa watu karibu 20,000 nchini Ethiopia.

‘Nia ya kufikia bahari’

Kwa upande mwingine, Waziri Mkuu wa ​​​​​​​Ethiopia amesema kuwa ameiomba Uturuki iwasaidie katika mchakato wao wa kutaka kutumia bahari, akieleza hilo kuwa eneo la msingi watakaloangazia katika mazungumzo yao na rais wa Uturuki.

Abiy alisema katika mkutano huo wa pamoja na waandishi wa habari kuwa alijadili nia ya Ethiopia ya kutaka “kufikia bahari” na kiongozi wa Uturuki na kupongeza majadiliano muhimu na yenye tija kuhusu suala hilo.

Ethiopia, ambayo ni nchi isiyokuwa na bahari tangu uhuru wa Eritrea 1993, imekuwa ikieleza kuwa kufikia bahari kama suala la kipaumbele kimkakati.

Ziara ya Erdogan ni ishara ya ziara ya ngazi ya juu ikiwajumuisha mawaziri wa mambo ya nje na ulinzi wa Uturuki, miongoni mwa wengine, na imekuja wakati nchi hizo mbili zikitaka kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na kisiasa hasa wakiadhimisha karne moja ya ushirikiano ulioanza 1926.

Viongozi hao walijadili kupanua ushirikiano wao wa kibiashara,huku maafisa wa Ethiopia wakisema pande zote mbili zinataka kuongeza kiwango cha biashara kisiwe chini ya dola bilioni $1.

Abiy pia alihimiza uwekezaji zaidi wa makampuni ya Uturuki nchini Ethiopia, nchi ambayo tayari ina mkusanyiko mkubwa zaidi wa wafanyabiashara wa Uturuki Kusini mwa jangwa la Sahara, hasa katika sekta ya viwanda na ujenzi.

Pande zote mbili pia zilijadili ushirikiano katika majukwaa ya kimataifa, ikiwemo majadiliano yanayohusiana na COP31, ambayo itafanyika nchini Uturuki, alafu mkutano unaofuata ufanyike nchini Ethiopia mwakani.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Uturuki inapanua utaalam wa reli, kutoa mafunzo kwa wafanyakazi Afrika, Asia
Erdogan: Uturuki inaendelea kutafuta amani ya kanda licha hofu iliyopo ulimwenguni
Rais wa Uturuki ateuwa Waziri mpya wa Katiba na Mambo ya Ndani katika mabadiliko ya Baraza la Mawazi
Fidan wa Uturuki akataa mashambulizi ya anga kama njia ya kubadilisha uongozi wa Iran
Makamu wa Rais wa Uturuki akutana na balozi wa Brazil
Idadi ya watu nchini Uturuki yafikia milioni 86 kwa mwaka 2025
Uturuki yalaani shambulizi la RSF nchini Sudan
Matetemeko ya ardhi ya Uturuki 2023 yalisababisha hasara ya dola bilioni 250: Erdogan
Fidan wa Uturuki akutana na Kamishna wa Maswala ya Wanachama wa EU, kujadili masuala ya ushirikiano
Rais wa Uturuki aadhimisha kumbukumbu ya miaka 3 ya tetemeko la ardhi
Uturuki imelaani shambulizi la kigaidi nchini Nigeria lililoua takriban watu 170
Uturuki kuimarisha uwepo wake wa kijeshi kuisaidia Somalia kupambana na ugaidi
Uturuki na Saudi Arabia kuimarisha ushirikiano wa ulinzi na uwekezaji katika ndege za kivita za KAAN
Mke wa Rais wa Uturuki amekutana na mwenzake wa Misri jijini Cairo
Erdogan na Sisi waimarisha ushirikiano kati ya Uturuki na Misri wajadili Gaza na migogoro ya kikanda
Kikao cha mwisho cha Jukwaa la Biashara kati ya Uturuki na Misri chafunguliwa jijini Cairo
Erdogan na Mwanamfalme wa Saudia waunga mkono umoja wa Somalia, wajadili masuala ya kikanda
Rais wa Uturuki Erdogan akutana na Mwanamfalme wa Saudia Mohammed bin Salman jijini Riyadh
Uturuki yapongeza hatua zinazoimarisha amani, utulivu nchini Syria: Erdogan
Uturuki yasema kuongeza mamlaka ya ujumbe wa amani wa UN bila kushirikisha Kupro ya Uturuki ni kosa