| Swahili
UTURUKI
1 dk kusoma
Ujerumani inaunga mkono nafasi ya Uturuki katika usalama wa Ulaya
Kufuatia mazungumzo yaliyofanyika Berlin, Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani, Pistorius, amesema kuwa Ujerumani inaitambua Uturuki kama mshirika muhimu na inapanga kuimarisha zaidi ushirikiano wa mataifa mawili katika masuala ya ulinzi.
Ujerumani inaunga mkono nafasi ya Uturuki katika usalama wa Ulaya
Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani Boris Pistorius akiwasili kwa mkutano wa baraza la mawaziri mjini Berlin, Ujerumani Januari 14, 2026. / / Reuters
15 Januari 2026

Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani, Boris Pistorius, alisifu mchango mkubwa wa Uturuki katika usalama wa Ulaya kufuatia mazungumzo ya Jumatano na mwenzake wa Uturuki, Yasar Guler, yaliyofanyika Berlin, Ujerumani.

Mawaziri hao walijadili maendeleo ya hivi karibuni nchini Ukraine na Syria, ushirikiano wa ulinzi kati ya nchi hizo mbili, pamoja na maandalizi ya mkutano ujao wa NATO, wakati wa mikutano uliyofanyika katika makao makuu ya wizara ya ulinzi.

“Ujerumani inaithamini Uturuki kama mshirika muhimu anayetoa mchango wa msingi katika usalama wa Ulaya,” Pistorius alisema katika taarifa ya wizara.

“Vikosi vya jeshi la Uturuki vinachangia kwa kiasi kikubwa kulinda ukingo wa kusini wa muungano.”

Pistorius alisisitiza maslahi ya pamoja kati ya washirika wa NATO na kusema kuwa ushirikiano wa ulinzi wa pande mbili unapaswa kuimarishwa zaidi, zaidi ya mifumo iliyopo ya muungano.

“Ujerumani na Uturuki zina uhusiano uliokomaa wa usalama na ulinzi ndani ya muungano. Aidha, tunataka kuimarisha zaidi ushirikiano wetu na Uturuki,” alisema.

Pia mawaziri hao walijadili ajenda za mkutano wa NATO utakaofanyika Ankara mwezi Julai, kwa mujibu wa taarifa hiyo. Mkutano huo utashughulikia kwa kina masuala ya NATO katika kukabiliana na vitisho vya kiusalama, ili kuhakikisha muungano huo unajiandaa kukabiliana na hatari kutoka pande zote.

CHANZO:Anadolu Agency
Soma zaidi
Erdogan: Kwa Israel kutambua Somaliland hakutamfaidi yeyote
Rais wa Uturuki awasili Ethiopia kwa ziara rasmi
Emine Erdogan awatuza wasukuma mabadiliko wakati wa makala ya 7 ya tuzo za TRT World
Rais wa Uturuki aelekea Ethiopia kwa ziara ya kikazi
Waziri Mkuu wa Somalia apongeza uchimbaji mafuta wa 'kihistoria' baharini na Uturuki
Uturuki inapanua utaalam wa reli, kutoa mafunzo kwa wafanyakazi Afrika, Asia
Erdogan: Uturuki inaendelea kutafuta amani ya kanda licha hofu iliyopo ulimwenguni
Rais wa Uturuki ateuwa Waziri mpya wa Katiba na Mambo ya Ndani katika mabadiliko ya Baraza la Mawazi
Fidan wa Uturuki akataa mashambulizi ya anga kama njia ya kubadilisha uongozi wa Iran
Makamu wa Rais wa Uturuki akutana na balozi wa Brazil
Idadi ya watu nchini Uturuki yafikia milioni 86 kwa mwaka 2025
Uturuki yalaani shambulizi la RSF nchini Sudan
Matetemeko ya ardhi ya Uturuki 2023 yalisababisha hasara ya dola bilioni 250: Erdogan
Fidan wa Uturuki akutana na Kamishna wa Maswala ya Wanachama wa EU, kujadili masuala ya ushirikiano
Rais wa Uturuki aadhimisha kumbukumbu ya miaka 3 ya tetemeko la ardhi
Uturuki imelaani shambulizi la kigaidi nchini Nigeria lililoua takriban watu 170
Uturuki kuimarisha uwepo wake wa kijeshi kuisaidia Somalia kupambana na ugaidi
Uturuki na Saudi Arabia kuimarisha ushirikiano wa ulinzi na uwekezaji katika ndege za kivita za KAAN
Mke wa Rais wa Uturuki amekutana na mwenzake wa Misri jijini Cairo
Erdogan na Sisi waimarisha ushirikiano kati ya Uturuki na Misri wajadili Gaza na migogoro ya kikanda