| Swahili
UTURUKI
1 dk kusoma
Ujerumani inaunga mkono nafasi ya Uturuki katika usalama wa Ulaya
Kufuatia mazungumzo yaliyofanyika Berlin, Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani, Pistorius, amesema kuwa Ujerumani inaitambua Uturuki kama mshirika muhimu na inapanga kuimarisha zaidi ushirikiano wa mataifa mawili katika masuala ya ulinzi.
Ujerumani inaunga mkono nafasi ya Uturuki katika usalama wa Ulaya
Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani Boris Pistorius akiwasili kwa mkutano wa baraza la mawaziri mjini Berlin, Ujerumani Januari 14, 2026. / / Reuters
15 Januari 2026

Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani, Boris Pistorius, alisifu mchango mkubwa wa Uturuki katika usalama wa Ulaya kufuatia mazungumzo ya Jumatano na mwenzake wa Uturuki, Yasar Guler, yaliyofanyika Berlin, Ujerumani.

Mawaziri hao walijadili maendeleo ya hivi karibuni nchini Ukraine na Syria, ushirikiano wa ulinzi kati ya nchi hizo mbili, pamoja na maandalizi ya mkutano ujao wa NATO, wakati wa mikutano uliyofanyika katika makao makuu ya wizara ya ulinzi.

“Ujerumani inaithamini Uturuki kama mshirika muhimu anayetoa mchango wa msingi katika usalama wa Ulaya,” Pistorius alisema katika taarifa ya wizara.

“Vikosi vya jeshi la Uturuki vinachangia kwa kiasi kikubwa kulinda ukingo wa kusini wa muungano.”

Pistorius alisisitiza maslahi ya pamoja kati ya washirika wa NATO na kusema kuwa ushirikiano wa ulinzi wa pande mbili unapaswa kuimarishwa zaidi, zaidi ya mifumo iliyopo ya muungano.

“Ujerumani na Uturuki zina uhusiano uliokomaa wa usalama na ulinzi ndani ya muungano. Aidha, tunataka kuimarisha zaidi ushirikiano wetu na Uturuki,” alisema.

Pia mawaziri hao walijadili ajenda za mkutano wa NATO utakaofanyika Ankara mwezi Julai, kwa mujibu wa taarifa hiyo. Mkutano huo utashughulikia kwa kina masuala ya NATO katika kukabiliana na vitisho vya kiusalama, ili kuhakikisha muungano huo unajiandaa kukabiliana na hatari kutoka pande zote.

CHANZO:Anadolu Agency
Soma zaidi
Makamu wa Rais wa Uturuki akutana na balozi wa Brazil
Idadi ya watu nchini Uturuki yafikia milioni 86 kwa mwaka 2025
Uturuki yalaani shambulizi la RSF nchini Sudan
Matetemeko ya ardhi ya Uturuki 2023 yalisababisha hasara ya dola bilioni 250: Erdogan
Fidan wa Uturuki akutana na Kamishna wa Maswala ya Wanachama wa EU, kujadili masuala ya ushirikiano
Rais wa Uturuki aadhimisha kumbukumbu ya miaka 3 ya tetemeko la ardhi
Uturuki imelaani shambulizi la kigaidi nchini Nigeria lililoua takriban watu 170
Uturuki kuimarisha uwepo wake wa kijeshi kuisaidia Somalia kupambana na ugaidi
Uturuki na Saudi Arabia kuimarisha ushirikiano wa ulinzi na uwekezaji katika ndege za kivita za KAAN
Mke wa Rais wa Uturuki amekutana na mwenzake wa Misri jijini Cairo
Erdogan na Sisi waimarisha ushirikiano kati ya Uturuki na Misri wajadili Gaza na migogoro ya kikanda
Kikao cha mwisho cha Jukwaa la Biashara kati ya Uturuki na Misri chafunguliwa jijini Cairo
Erdogan na Mwanamfalme wa Saudia waunga mkono umoja wa Somalia, wajadili masuala ya kikanda
Rais wa Uturuki Erdogan akutana na Mwanamfalme wa Saudia Mohammed bin Salman jijini Riyadh
Uturuki yapongeza hatua zinazoimarisha amani, utulivu nchini Syria: Erdogan
Uturuki yasema kuongeza mamlaka ya ujumbe wa amani wa UN bila kushirikisha Kupro ya Uturuki ni kosa
Televisheni ya kitaifa ya Uturuki TRT yaadhimisha miaka 58 ya utangazaji
Iran iko 'tayari' kwa 'makubaliano ya nyuklia ya haki na ya usawa': mwanadiplomasia mkuu
Uturuki iko tayari kusuluhisha mvutano kati ya Marekani na Iran: Erdogan amwambia Pezeshkian
Uturuki inakuwa moja ya kituo chenye ushawishi wa kisiasa duniani: rais wa Uzbekistan