| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Mahakama Kuu ya Kenya: Mchakato wa kumuondoa Gachagua madarakani ulifuata Sheria
Mahakama Kuu ya Kenya imeidhinisha kuondolewa madarakani kwa Gachagua, pamoja na kuamuru kulipwa fidia ya shilingi milioni 50 za Kenya kwa ukiukwaji wa haki zake.
Mahakama Kuu ya Kenya: Mchakato wa kumuondoa Gachagua madarakani ulifuata Sheria
Hata hivyo Gachagua bado ana haki ya kukata rufaa katika Mahakama ya Rufaa.

Mahakama Kuu ya Kenya imethibitisha uamuzi wa kumwondoa madarakani aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua, ikiamua kwamba mchakato wa kubanduliwa kwake ulikuwa wa kikatiba na halali.

Katika uamuzi uliotolewa na jopo la majaji watatu, mahakama ilisema Bunge la Kitaifa na Seneti zilifuata mamlaka yao ya kikatiba zilipopitisha uamuzi wa kumwondoa Gachagua madarakani mwaka 2024. Majaji hao waliamua kwamba masharti ya kikatiba ya kuondolewa madarakani kwa Gachagua yalizingatiwa na kwamba uamuzi huo haukuwa batili.

Hata hivyo, mahakama hiyo pia ilibaini kuwa kulikuwa na ukiukwaji wa baadhi ya haki za kikatiba za Gachagua, hususan haki ya kusikilizwa.

Kutokana na ukiukwaji huo, mahakama ilitoa tamko kwamba haki zake zilivunjwa na ikaamuru apewe fidia ya Shilingi milioni 50 za Kenya.

Majaji hao walisisitiza kuwa ingawa kuondolewa kwake ilikuwa halali na itaendelea kubaki kuwa na nguvu kisheria, ukiukwaji wa haki za kikatiba hauwezi kupuuzwa, hivyo fidia ilitolewa chini ya Katiba ya Kenya.

Gachagua alikuwa amepinga kuondolewa kwake akidai kuwa mchakato huo ulikuwa wa kisiasa, uliokiuka taratibu, na kwamba hakupata nafasi ya kutosha kujitetea. Mahakama ilikataa hoja za kubatilisha kuondolewa kwake madarakani, lakini ikaunga mkono madai ya ukiukwaji wa baadhi ya haki zake.

Mahakama Kuu ya Kenya imethibitisha uamuzi wa kumwondoa madarakani aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua, ikiamua kwamba mchakato wa kubanduliwa kwake ulikuwa wa kikatiba na halali.

Hata hivyo Gachagua bado ana haki ya kukata rufaa katika Mahakama ya Rufaa.

Soma zaidi
Waandamanaji nchini Afrika Kusini wanavamia nyumba hadi nyumba kuwasaka wahamiaji
Morocco yaahidi kujiimarisha zaidi baada ya kutolewa Kombe la Dunia
Benki ya Dunia: Wakenya milioni 2.4 wako hatarini kutumbukia kwenye umaskini
Aliyekuwa Kiongozi Mkuu wa Iran, Ali Khamenei azikwa, huku waombolezaji waapa kulipiza kisasi
Urusi kuisaidia Msumbiji kupambana na ugaidi
Tanzania: Watu 130 wakamatwa kwa kuhamasisha vitendo vya kihalifu
Marekani yashambulia daraja muhimu la reli linalounganisha Iran, China na Urusi
Morocco iko imara kuliko Paraguay: Kocha wa Ufaransa Deschamps
Vifo vya Ebola vyafikia 600 nchini DRC huku maambukizi yakiripotiwa katika jimbo jipya
CCM na ACT-Wazalendo wamaliza mgogoro wa kisiasa Zanzibar
Somalia yapongeza upatanishi wa Uturuki baada ya upinzani kukubali mazungumzo ya katiba
Iran yaionya Marekani baada ya mashambulizi mapya, yasema ni Iran pekee itakayoamua hatima ya Hormuz
Tanzania yanunua zaidi ya tani 28 za dhahabu ili kuongeza akiba ya fedha za kigeni
Vita vya Sudan: Watu 10 wameuawa katika shambulio la droni kwenye sherehe ya harusi
Wafanyakazi wa afya nchini DR Congo wagoma huku vifo vya Ebola vikikaribia 600
Polisi na jeshi la Afrika Kusini wawakamata zaidi ya wachimbaji madini haramu 200
Rais Mnangagwa apitisha sheria ya kumuongezea muda wa kukaa madarakani
Ufaransa yawaondoa wanadiplomasia kutoka Burkina Faso.
Saba Saba: Polisi wapiga marufuku maandamano katika kumbukumbu ya maandamano ya Kenya.
Wakulima wa Uganda wafungua kesi dhidi ya mradi wa bomba la mafuta unaoungwa mkono na Uingereza