| Swahili
UTURUKI
1 dk kusoma
Uturuki yalaani shambulizi la RSF nchini Sudan
Kulingana na taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki, tukio hilo ni ukiukwaji mkubwa wa haki za kibinadamu na ulinzi wa uhai wa binadamu na mali zao.
Uturuki yalaani shambulizi la RSF nchini Sudan
Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki yalaani shambulizi la RSF nchini Sudan./Picha:Wengine
8 Februari 2026

Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki imelaani vikali shambulizi lililofanywa na vikosi vya RSF vya nchini Sudan, kwenye gari lililokuwa limebaba watu wasio na makazi, katika eneo la Jimbo la Kordofan.

Kulingana na taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki, tukio hilo ni ukiukwaji mkubwa wa haki za kibinadamu na ulinzi wa uhai wa binadamu na mali zao.

“Tumesikitishwa na vifo vya watu wengi kufutia shambulizi lililofanywa na RSF, likilenga gari lililokuwa limebeba awatu wasio na makazi,” ilisomeka sehemu ya taarifa hiyo.

Vile vile, Uturuki imelaani vikali mashambulizi dhidi ya raia wasio na hatia, ikitaka kuwepo na ulinzi wakati wa kusafirisha binadamu na misaada kwenye maeneo yaliyokumbwa na machafuko.

Februari 7, shambulizi la ndege isiyokuwa na rubani ya wapiganaji wa Sudan, lililenga gari lililokuwa limebeba familia zilizokuwa zimeondoka kwenye makazi yao katikati mwa Sudan, kuua watu wasiopungua 24, ikiwemo watoto wanane, kulingana na taasisi moja ya madaktari.

Shambulio hilo lilitokea karibu na mji wa Rahad, katika jimbo la Kordofan Kaskazini.

Gari hilo lililokuwa likisafirisha watu waliokimbia makazi yao kutokana na vita huko eneo la Dubeiker Kordofan Kaskazini.

Miongoni mwa waliofariki walikuwa watoto wawili wachanga.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Rais wa Uturuki aadhimisha kumbukumbu ya miaka 3 ya tetemeko la ardhi
Uturuki imelaani shambulizi la kigaidi nchini Nigeria lililoua takriban watu 170
Uturuki kuimarisha uwepo wake wa kijeshi kuisaidia Somalia kupambana na ugaidi
Uturuki na Saudi Arabia kuimarisha ushirikiano wa ulinzi na uwekezaji katika ndege za kivita za KAAN
Mke wa Rais wa Uturuki amekutana na mwenzake wa Misri jijini Cairo
Erdogan na Sisi waimarisha ushirikiano kati ya Uturuki na Misri wajadili Gaza na migogoro ya kikanda
Kikao cha mwisho cha Jukwaa la Biashara kati ya Uturuki na Misri chafunguliwa jijini Cairo
Erdogan na Mwanamfalme wa Saudia waunga mkono umoja wa Somalia, wajadili masuala ya kikanda
Rais wa Uturuki Erdogan akutana na Mwanamfalme wa Saudia Mohammed bin Salman jijini Riyadh
Uturuki yapongeza hatua zinazoimarisha amani, utulivu nchini Syria: Erdogan
Uturuki yasema kuongeza mamlaka ya ujumbe wa amani wa UN bila kushirikisha Kupro ya Uturuki ni kosa
Televisheni ya kitaifa ya Uturuki TRT yaadhimisha miaka 58 ya utangazaji
Iran iko 'tayari' kwa 'makubaliano ya nyuklia ya haki na ya usawa': mwanadiplomasia mkuu
Uturuki iko tayari kusuluhisha mvutano kati ya Marekani na Iran: Erdogan amwambia Pezeshkian
Uturuki inakuwa moja ya kituo chenye ushawishi wa kisiasa duniani: rais wa Uzbekistan
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran kuelekea Uturuki kwa mazungumzo muhimu siku ya Ijumaa
Uturuki yasema kujiunga na EU haiwezekani katika mazingira ya sasa ya kisiasa
Mawaziri wa mambo ya nje wa Uturuki, Nigeria kujadili biashara, ulinzi
Mkuu wa ujasusi wa Uturuki akutana na ujumbe wa Hamas mjini Istanbul
Mapambano dhidi ya ugaidi wa Daesh yanazidi kuwa na nguvu: Erdogan