| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Wananchi waelimishwe kuhusu umuhimu wa kuandikishana mikataba ya ardhi-Wazri Mkuu wa Tanzania
Ushauri huo umetolewa kufuatia kuongezeka kwa wimbi la migogoro katika sekta ya ardhi.
Wananchi waelimishwe kuhusu umuhimu wa kuandikishana mikataba ya ardhi-Wazri Mkuu wa Tanzania
Waziri Mkuu wa Tanzania Mwigulu Nchemba ametaka viongozi kutoa elimu kwa wananchi kuhusu mikataba ya ardhi. Picha/PMO / TRT Afrika Swahili

Waziri Mkuu wa Tanzania Mwigulu Nchemba amewataka viongozi nchini humo kuwaelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa kuandikishana mikataba pindi wanapopeana ardhi badala ya kufanya hivyo kwa kuaminiana.

"Viongozi mliopo hapa waambieni wananchi hivi sasa masuala ya ardhi wasifanye kwa kuaminiana, wawe wanaandikishana kwa mikataba na tena katika ofisi za kijiji ili watambulike," amesema.

Kauli hiyo ametoa Juni 7, 2026 alipokuwa akizungumza na viongozi wa kada mbalimbali wa mkoa wa Iringa katika kikao cha majumuisho ya ziara zake.

"Ninawasihi wananchi tusiogope kurasimisha mambo yetu kwa sababu uaminifu unapungua. Tunaporasmisha, tunaepusha migogoro siku za usoni," amesisitiza.

Ushauri huo umetolewa kufuatia kuongezeka kwa wimbi la migogoro katika sekta ya ardhi.

Wakati huo huo, amewataka viongozi wanapotaka kufanya uendelezaji wowote nao pia wahakikishe wanawapa wananchi husika mikataba ili kulinda haki yao.

"Tusichukue maeneo ya watu bila kuwalipa fidia. Kama kuna uendelezaji ni lazima kuwe na mikataba rasmi. Wananchi wa eneo husika wapewe barua za kuonesha utwaaji huo wakati wakisubiri fedha za fidia zipatikane. Liwe ni eneo limetengwa kwa uwekezaji, ujenzi wa barabara au shule, watu wapewe barua. Ardhi ni jambo rasmi ndiyo sababu presha ya matumizi inazidi kuongezeka," alisema.

Soma zaidi
Misri, Qatar wasisitiza utekelezaji wa makubaliano ya awamu ya kwanza ya kusitisha mapigano Gaza
DRC kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Chile nchini Ufaransa baada ya marufuku ya Hispania
Afrika Kusini yaishutumu Ghana kufanya 'mbwembwe za umma' wakati wa kurudisha raia wake
Utafiti wa miaka mingi wa kutafuta mnyama anayeeneza virusi vya Ebola
Boko Haram yawaachilia mamia ya watu waliotekwa nyara nchini Nigeria
Askofu wa Msumbiji afariki baada ya kupigwa risasi nyumbani kwake
Mauritius inazuia kuingia kwa wasafiri kutoka nchi zilizokumbwa na Ebola
Utamaduni uliokosea? Jinsi usimamizi wa AI unatishia Usanii wa kimila wa Kiafrika
Janga la Ebola: Wafanyabiashara wapata hasara kubwa katika mpaka wa Uganda-DRC
Mchekeshaji wa Kenya Eric Omondi akamatwa kwa maandamano kupinga kupanda bei ya mafuta
Ebola inaenea 'kwa kasi' huku maambukizi 71 mapya yakithibitishwa katika siku moja
Chama tawala cha Guinea chashinda kwa kishindo bungeni, uchaguzi wa manispaa
Mali yamfunga jela mwanadiplomasia wa Ufaransa kwa madai ya njama ya kuvuruga utulivu
Watu wasiopungua 49 wafariki kwa kiu katika jangwa la Sahara baada ya gari kuharibika Niger
Nigeria kuwasafirisha raia wake zaidi 1,000 kutoka Afrika Kusini
Kiwanda cha mafuta cha Dangote Nigeria chaongeza uwezo, chasafisha mapipa 700,000
Waandamanaji wavamia ofisi ya UN Libya
Mkuu wa Umoja wa Mataifa asikitishwa na ripoti za ghasia katika mji mkuu wa Somalia
Uturuki, Niger watia saini makubaliano ya ushirikiano baada ya mazungumzo ngazi ya urais
Afrika kuwa na mabilionea 10 tu zaidi katika kipindi cha miaka mitano ijayo