| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Rais wa Djibouti Guelleh awasilisha ombi la kugombea muhula wa sita
Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 77 anaruhusiwa kugombea tena baada ya bunge bunge mwaka jana kuondoa ukomo wa umri kikatiba kwa wagombea urais.
Rais wa Djibouti Guelleh awasilisha ombi la kugombea muhula wa sita
Rais Ismail Omar Guelleh amekuwa madarakani tangu 1999. / AA
tokea masaa 2

Rais wa Djibouti Ismail Omar Guelleh, ambaye amekuwa madarakani tangu 1999, amewasilisha rasmi ombi la kugombea muhula wa sita katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwezi Aprili, kulingana na Wizara ya Mambo ya Ndani.

Ombi la Guelleh liliwasilishwa siku ya Jumatatu na mkurugenzi wa kampeni yake, Abdallah Abdillahi Miguil, ambaye ni mwanachama mwandamizi wa Muungano unaoongoza serikali, UMP.

Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 77 anaruhusiwa kugombea tena baada ya bunge mwaka jana kuondoa ukomo wa umri kikatiba kwa wagombea urais.

Katiba ilikuwa tayari imebadilishwa 2010 kuondoa sheria ya mihula miwili pekee kwa urais.

Guelleh anagombea tena urais kupitia muungano wa vyama kadhaa vya kisiasa ambavyo vinaunga mkono serikali.

Mamlaka za Uchaguzi zinatarajiwa kutathmini maombi hayo kabla ya kutangaza orodha ya mwisho ya wagombea wanaoruhusiwa kwenye uchaguzi.

Kampeni za uchaguzi zinatarajiwa kuanza katika wiki chache zijazo.

CHANZO:TRT Afrika Swahili