| swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Msongamano katika mazishi ya Raila wasababisha watu kadhaa kujeruhiwa
Watu kumi na nane wamejeruhiwa wakati wa msongamano uliojitokeza katika uwanja wa Nyayo wakati wa mazishi ya kitaifa ya Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya, Raila Odinga, aliyefariki dunia wiki hii India akiwa na umri wa miaka 80.
Msongamano katika mazishi ya Raila wasababisha watu kadhaa kujeruhiwa
Msongamano ulitokea katika uwanja wa Nyayo uliopo jijini Nairobi, wakati umma ulipokuwa ukiuaga mwili wa Odinga.
17 Oktoba 2025

Wakenya wamejitokeza kwa wingi kuomboleza kifo cha Odinga tangu alipoaga dunia Jumatano, jambo linaloonyesha ushawishi mkubwa wa kiongozi huyo aliyeheshimiwa katika siasa za nchi hiyo ya Afrika Mashariki.

Msongamano ulitokea katika uwanja huo uliopo jijini Nairobi, wakati umma ulipokuwa ukiuaga mwili wa Odinga.

Shirika la Msalaba Mwekundu wa Kenya limesema tukio hilo "lilisababisha watu wengi kuhitaji huduma za dharura." Chanzo katika hospitali kuu ya rufaa nchini kilisema walipokea watu 18 waliokuwa wamejeruhiwa.

Maelfu ya watu wamejaza uwanja wa Nyayo ambapo jeneza la Odinga lilifunikwa na bendera ya taifa kwa ajili ya ibada ya Kanisa la Anglican. Watu walikuwa wakimwimbia nyimbo na kuonyesha picha za Odinga, huku wengine wakibeba matawi, ambayo ni ishara ya amani na mshikamano katika mila za Kenya.

Kulikuwa na usalama mkali uwanjani baada ya watu wanne kuripotiwa kufariki dunia wakati wa kuuaga mwili wa Odinga siku ya Alhamisi, wakati polisi walipojaribu kudhibiti umati mkubwa katika uwanja Kasarani.

Angalau watu 10 walijeruhiwa katika tukio la Alhamisi baada ya polisi kufyatua risasi na kutumia mabomu ya machozi dhidi ya umati uliokuwa ukijaribu kufikia eneo la jeneza.

CHANZO:AP
Soma zaidi
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti
Nigeria yaanzisha uchunguzi baada ya kukamata kilo 1,000 za kokeini yenye thamani ya $235M
Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam
Mtoto wa Gaddafi aachiliwa huru baada ya miaka kumi gerezani
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Zaidi ya mataifa 20 yanalaani ukatili wa RSF nchini Sudan, na kutaka kukomeshwa kwa ghasia
Rais wa Misri, afisa mkuu wa usalama wa Urusi kujadili ushirikiano wa kijeshi
Maelfu ya wananchi wanashikiliwa katika hali mbaya sana katika Al Fasher, Sudan: madaktari
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aghairi ziara iliyopangwa nchini Kenya
‘Mauaji ya waandamanaji ni chukizo mbele za Mungu’
Jeshi la Sudan lazima shambulio la RSF katika mji wa Babnousa huko Kordofan Magharibi
Majeshi ya Somalia yawaua viongozi watatu wakuu wa Al Shabaab
Rwanda, DRC zaanzisha mfumo wa ushirikiano wa kiuchumi huku kukiwa na mazungumzo ya amani
RSF yazika miili katika makaburi ya halaiki, inachoma wengine ili 'kuficha ushahidi wa mauaji
Wananchi katika Al Fasher, Sudan, wanakabiliwa na ukatili 'wa kiwango kisichoweza kuaminika' — UN
Chama tawala nchini Djibouti kimemteua Rais Guelleh kwa muhula wa sita
Amaan Golugwa akamatwa huku polisi Tanzania ikiwasaka viongozi wa upinzani kufuatia maandamano