| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Jamhuri ya Congo yafanya Uchaguzi Mkuu
Rais wa sasa Denis Sassou Nguesso mwenye umri wa miaka 82 anachuana na wagombea wengine sita.
Jamhuri ya Congo yafanya Uchaguzi Mkuu
Rais wa sasa Dennis Sassou Nguesso anawania tena muhula wake wa mwisho iwapo atashinda. / Reuters
15 Machi 2026

Jamhuri ya Congo inafanya Uchaguzi wake Mkuu hii leo Machi 15, 2026, kumchagua rais.
Zoezi la kupiga kura lilianza saa moja asubuhi kwa saa za ndani (0600 GMT) na litakamilika saa kumi na mbili jioni.

Zaidi ya Wacongo milioni 3.2 wamejiandikisha kupiga kura.

Rais wa sasa Denis Sassou Nguesso mwenye umri wa miaka 82 anachuana tena na iwapo atashinda basi itakuwa muhula wake wa tano mtawalia.

Kuna wagombea sita katika mchuano huyo, ingawa wachambuzi wanasema hakuna anayeonekana kuwa mpinzani mkubwa.

"Upinzani umegawanyika na hauna mtu madhubuti," alisema Remadji Hoinathy wa Taasisi ya Mafunzo ya Usalama yenye makao yake makuu mjini Pretoria. "Kunaweza kuwa na uchovu kati ya wapiga kura, lakini hiyo haitaathiri nafasi ya Sassou."

Viongozi wawili wa upinzani nchini humo wanasalia gerezani, huku wengine wakiwa uhamishoni.

Vyama kadhaa vya upinzani vimesusia uchaguzi huo, kwa madai mchakato huo hauendeshwi kwa usawa.

Sassou alichukua mamlaka ya nchi hiyo inayozalisha mafuta ya Afrika ya Kati mwaka 1979 na ametawala kwa mfululizo tangu wakati huo, isipokuwa kwa mapumziko ya miaka mitano katika miaka ya 1990.

Baadhi ya raia wa Congo wanasema wanaona nafasi ndogo ya mabadiliko.

Waziri Mkuu Anatole Collinet Makosso amepuuzilia mbali shutuma za kuegemea upande wa Sassou, akisema kuwa vyombo vya uangalizi vya Congo vitahakikisha uchaguzi unakuwa wa wazi na wa haki.

Sassou amefanya kampeni akiahidi kuharakisha miradi ya maendeleo na kupanua upatikanaji wa elimu na mafunzo ya kitaaluma.

Uchumi wa Congo unaotegemea sana mafuta, umetulia katika miaka ya hivi karibuni baada ya kuzorota kwa muda mrefu, lakini asilimia 52 ya watu milioni 6.1 wa Congo wanaishi katika umaskini, kulingana na Benki ya Dunia.

Matokeo ya muda ya uchaguzi yanatarajiwa kutoka kati ya saa 48 hadi 72 baada ya upigaji kura kufungwa.

CHANZO:reuters
Soma zaidi
Mwakilishi Maalumu wa Jumuiya ya Madola Lazarus Chakwera ahitimisha ziara yake nchini Tanzania
Kenya yaomba msaada wa haraka kutoka Benki ya Dunia huku ikipunguza VAT
Wadau wajadili fursa za uwekezaji katika Kongamano la Biashara linaloendelea Kigoma, Tanzania
Mbunge Tanzania ataka sekta binafsi iruhusiwe uzalishaji wa nishati ya umeme
Kampuni ya BP yashtakiwa Kenya kufuatia madai ya uchafuzi mazingira kutokana na uchimbaji mafuta
Mashirika ya ndege ya Nigeria yatishia kusitisha huduma kuanzia Aprili 20 kutokana na bei ya mafuta
Somalia yashtumu uteuzi wa balozi wa Israel katika eneo lililojitenga la Somaliland
Uganda inasema inahitaji zaidi ya Dola bilioni moja kusambaza umeme nchini kote
Afrika Kusini yampa kifungo cha miaka mitano jela Julius Malema kwa kufyatua risasi
DRC inaanzisha hifadhi ya kimkakati ya kobalti na madini mengine
Afrika Kusini yamkamata mwanaharakati wa Benin Kemi Seba kwa tuhuma za uchochezi
Burkina Faso yafuta takriban asasi 100 za kiraia
Rais wa Cameroon anasema dunia inahitaji 'ujumbe wa amani' wa Papa
Jeshi la Tanzania latangaza nafasi ajira
Raia wa China ahukumiwa jela kwa kusafrisha mchwa kutoka Kenya kinyume cha sheria
Iran yatishia kuzuia usafiri wa meli katika Bahari ya Shamu ikiwa vikwazo vya Marekani vitaendelea
Marie-Louise Eta: Mwanamama aliyepewa mikoba Bundesliga
Mamia wajitokeza Afrika Kusini kabla ya hukumu ya kifungo cha mwanasiasa Malema
Wasichana ndio waathirika wakubwa zaidi katika vita vilivyosahaulika vya Sudan
Bei ya mafuta yapanda Kenya huku usambazaji ukisuasua