| Swahili
UTURUKI
3 dk kusoma
Uturuki yakumbuka miaka 10 ya jaribio la mapinduzi
Maadhimisho hayo yatafanyika katika bustani ya Millet jijini Ankara, siku ya Jumatano, yakihudhuriwa na Rais Recep Tayyip Erdogan.
Uturuki yakumbuka miaka 10 ya jaribio la mapinduzi
Madhimisho hayo, yataongozwa na kauli mbiu ya Nia Yetu, Ushindi Wetu, kulingana na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Uturuki Burhanettin Duran.

Uturuki itaadhimisha miaka 10 tangu kutokea kwa jaribio la mapinduzi la Julai 15, 2016.

Madhimisho hayo, yataongozwa na kauli mbiu ya Nia Yetu, Ushindi Wetu, kulingana na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Uturuki Burhanettin Duran.

Maadhimisho hayo yatafanyika katika bustani ya Millet jijini Ankara, siku ya Jumatano, yakihudhuriwa na Rais Recep Tayyip Erdogan.

“Maadhimisho hayo yatahudhuriwa na Rais Recep Tayyip Erdogan, ambapo tutawakumbuka mashahidi wetu kwa sala na shukrani, tukirudia ahadi ya kuwa hakuna atakayekuwa juu ya nia ya taifa,” alisema Duran.

Kupitia chapisho lililowekwa kwenye mtandao wa kijamii wa NSosyal wa Uturuki, Duran alisema tukio hilo litakukumbuka ujasiri wa umma dhidi ya jaribio hilo lililolenga kutia dosari demokrasia na utawala wa nchi.

Kulingana na Duran, ujasiri wa Julai 15 utaendelea kuishi mioyoni mwa Waturuki.

Jaribio lililoshindwa na mapinduzi hayo, liligharimu maisha ya watu 252 na kujeruhi wengine 2,734, likiongozwa na kiongozi wa FETO, Fethulla Gulen.

Kikundi hicho, kilitumia mwamvuli wa kidini kujipenyeza katika taasisi mbalimbali, ikiwemo Jeshi la Ulinzi la Uturuki, na kujaribu kuchukua madaraka kupitia mapinduzi.

Kabla ya jaribio hilo, kikundi cha FETO kiliendesha operesheni mbalimbali dhidi ya serikali, ikiwemo kumwita aliyekuwa mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (MIT), Hakan Fidan kwa mahojiano.

Kikundi hicho kiliendeleza vuguvugu lake, mara baada ya ushindi wa chama cha AK, kufuatia uchaguzi wa Novemba 1, 2015.

Kiongozi wa kikundi hicho, Fetullah Gulen, alitumia televisheni kutangaza jaribio la mapinduzi hayo.

Jaribio lawekwa wazi

Saa chache kabla ya jaribio hilo, meja wa kijeshi ndani ya jeshi la anga la Uturuki, aliifahamisha MIT, kuwa FETO walikuwa wanajaribu kumuweka kizuizini Fidan.

Taarifa hizo zilimfikia aliyekuwa Kaimu Mnadhimu Mkuu, Jenerali Yasar Guler, ambaye alimfikishia habari Mkuu wa Majeshi, Jenerali Hulusi Akar.

Akar alitoa amri ya ngome ya jeshi la anga kujiimarisha, ikiwemo kufunga anga la kudhibiti shughuli za kijeshi.

Magari ya kijeshi yalisambazwa Ankara, ambako wapinga mapinduzi walikuwa wameyadhibiti.

Sajini taji Bulent Aydin, alikuwa mtu wa kwanza kuuawa katika jaribio hilo, katika makao makuu ya jeshi.

Ndege za F-16 zilionekana zikiruka chini chini jijini Ankara, huku wanajeshi wakifunga daraja la Bosphorus na Msikiti wa Fatih Sultan Mehmet wa jijini Istanbul.

Magaidi wa FETO waliishambulia kwa mabomu Idara ya Operesheni Maalumu ya Polisi Anga na Idara ya Operesheni Maalumu iliyoko Golbasi, Ankara na kushambulia kituo cha MIT, pamoja na kuvamia chombo cha serikali cha TRT, na kuwataka watangazaji kutangaza mapinduzi hayo.

Ilipofika usiku wa Julai 16, Rais Recep Tayyip Erdogan alijitokeza kwenye kituo cha CNN Turk na kuwaomba wananchi kuingia mitaani, na kuiokomboa nchi yao.

Vuguvugu hilo liliendelea mpaka asubuhi, kabla ya waziri mkuu wa wakati huo, Yildirim kutangaza kuwa jaribio hilo kuwa limedhibitiwa.

Kulingana na mamlaka za Uturuki, Gulen ambaye aliasisi taasisi hiyo kwenye miaka ya 1960 na kukimbilia Marekani mwaka 1999, alielekeza mapinduzi ya Julai 15, akiwa jijini Pennsylvania.

Licha ya Uturuki kuwasilisha ombi la kumrudisha Gulen, bado Marekani ilisita kufanya hivyo.

Gulen alifariki dunia Oktoba 20, 2024 katika hospitali ya Mtakatifu Luka jijini Pennsylvania, nchini Marekani.

CHANZO:Anadolu Agency
Soma zaidi
Mashambulizi ya Israel yanatishia usalama wa Syria: Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki
Muswada wa “Uturuki Isiyo na Ugaidi” wafungua hatua muhimu katika kukomesha ugaidi: Erdogan
Mkuu wa mawasiliano wa Uturuki anasema Israel inahujumu juhudi za amani za Gaza
Uturuki inaweka historia kwa kusafirisha treni ya kwanza iliyotengenezwa nchini humo kwenda Afrika
Mkuu wa shirika la ujasusi wa Uturuki akutana na kiongozi wa Hamas kujadili mpango wa amani wa Gaza
Rais wa Uturuki na Mwana Mfalme wa Saudia wajadili usalama wa kikanda na mpango wa amani wa Gaza
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki na Kuwait wajadili yanayojiri katika kanda
Mkuu wa mawasiliano wa Uturuki anasema Israel inahujumu juhudi za kutafuta amani Gaza
Uturuki yalaani mashambulizi ya Israel huko Gaza, ikimtuhumu Netanyahu kwa kuhujumu juhudi za amani
Mpango wa 'Uturuki Isiyo na Ugaidi' kupata msukumo kupitia hatua za bunge: Erdogan
Uturuki na Iraq zasaini makubaliano ya kuongeza matumizi ya bomba la mafuta la Kirkuk-Ceyhan
Uturuki yamkamata gaidi wa FETO aliyekuwa akisakwa kwa jaribio la mwaka 2016 la kumuua Rais Erdogan
Sabiha Gokcen ya Istanbul yaongoza kwa ukuaji wa idadi ya abiria kati ya viwanja vya ndege Ulaya
Uturuki yaimarisha utoaji wa misaada duniani, ikisaidia nchi 85
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Sudan wakutana jijini Ankara
Trump apuuza pingamizi la Netanyahu kuhusu uuzaji wa ndege za kivita za F-35 kwa Uturuki
Erdogan wa Uturuki, Faye wa Senegal wajadili uhusiano, masuala ya dunia
Mwanadiplomasia wa Uturuki Fidan ajadili Kupro, Syria na masuala ya kanda na mkuu wa UN Guterres
Mwanadiplomasia mkuu wa Uturuki Fidan ajadili Cyprus, Syria na masuala ya kikanda na Guterres
Lilikuwa ni jambo la kifahari kuandaa mkutano wa NATO jijini Ankara, asema Erdogan