| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Julai 15 ilimaliza historia ya mapinduzi ya kijeshi nchini Uturuki: Spika wa Bunge
Numan Kurtulmus anasema kuwa upkaidi dhidi ya jaribio la mapinduzi la mwaka 2016 uliashiria 'ushindi wa demokrasia' na 'matakwa ya taifa'.
Julai 15 ilimaliza historia ya mapinduzi ya kijeshi nchini Uturuki: Spika wa Bunge
Kurtulmus alisema uongozi wa kisiasa, bunge, umma, misikiti na vyombo vya habari vilichukua nafasi muhimu katika kulishinda jaribio la mapinduzi. / / AA

Wananchi wa Uturuki walihitimisha historia ndefu ya mapinduzi ya kijeshi nchini humo kupitia upinzani wao dhidi ya jaribio la mapinduzi lililoshindwa la tarehe 15 Julai 2016, alisema Spika wa Bunge Numan Kurtulmus.

Akizungumza katika hafla ya kuadhimisha Siku ya Demokrasia na Umoja wa Kitaifa iliyofanyika katika Bunge siku ya Jumatano, Kurtulmuş alisema urithi mkubwa wa usiku huo ulikuwa “ushindi wa demokrasia” na “matakwa ya taifa.”

Alisema Uturuki imepitia mfululizo wa mapinduzi ya kijeshi yaliyoanzia mwishoni mwa kipindi cha Dola ya Ottoman na kuendelea katika historia ya jamhuri hiyo pamoja na mfumo wake wa siasa za vyama vingi.

“Wananchi waliamua hatima ya nchi yao asubuhi ya Julai 15 na waliondoa kabisa mienendo wa mapinduzi ya kijeshi kwenye historia,” alisema.

Kurtulmuş alisema uongozi wa kisiasa, Bunge, wananchi, misikiti na vyombo vya habari vilikuwa na nafasi muhimu katika kushinda jaribio hilo la mapinduzi.

Aliashiria wito wa Rais Recep Tayyip Erdogan kupitia televisheni uliowataka wananchi kujitokeza mitaani, akisema ujumbe huo uliwahamasisha mamilioni ya watu kupinga waliokuwa wakijaribu kupindua serikali.

Pia aliwasifu wabunge kutoka pande mbalimbali za kisiasa waliokusanyika ndani ya Bunge wakati jengo hilo lilipokuwa likishambuliwa, akisema uwepo wao ulionyesha nguvu ya demokrasia na umoja wa kitaifa.

Alisema matukio hayo yalionyesha umuhimu wa kuhakikisha taasisi za serikali haziwi eneo la ushawishi wa kundi lolote, huku akisisitiza umuhimu wa uwazi, taasisi imara, utawala wa sheria na mshikamano wa kitaifa.

Mnamo Julai 15, 2016, sehemu la kundi ndani ya Jeshi la Uturuki lililohusishwa na Shirika la Kigaidi la Fethullah (FETO) lilijaribu kupindua serikali iliyochaguliwa kidemokrasia nchini humo.

Waliopanga mapinduzi hayo walishambulia kwa mabomu Bunge na taasisi nyingine za serikali, na kuwafyatulia risasi raia, na kusababisha vifo vya watu 253 huku maelfu wengine wakijeruhiwa.

CHANZO:AA