| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Kombe la Dunia: Mchezaji wa Ghana Thomas Partey azuiwa kuingia Canada
Thomas Partey atakosa mechi ya ufunguzi ya Ghana katika Kombe la Dunia 2026 dhidi ya Panama.
Kombe la Dunia: Mchezaji wa Ghana Thomas Partey azuiwa kuingia Canada
Partey amekana madai ya ubakaji na unyanyasaji wa kingono. / / Reuters

Kiungo wa Ghana, Thomas Partey, hataichezea timu yake katika mechi dhidi ya Panama siku ya Jumatano baada ya ombi lake la viza ya kuingia Canada kukataliwa, kwa mujibu wa FIFA siku ya Ijumaa.

“FIFA inaweza kuthibitisha kwamba mchezaji Thomas Partey hataweza kusafiri kutoka kambi ya timu ya Ghana iliyoko Boston, Marekani, kwenda Canada kwa ajili ya mechi yao ya kwanza dhidi ya Panama siku ya Jumatano, tarehe 17 Juni, kwa sababu ombi lake la viza limekataliwa na serikali ya Canada,” FIFA ilisema katika taarifa yake kwa shirika la habari la Reuters.

“FIFA haihusiki na taratibu za uhamiaji za nchi mwenyeji, ikiwa ni pamoja na maamuzi kuhusu utoaji wa viza.”

Partey mwenye umri wa miaka 32, aliwahi kuchezea timu ya Arsenal, sasa anachezea timu ya Villarreal ya Hispania, anakabiliwa na madai ya ubakaji na unyanyasaji wa kingono nchini Uingereza. Hata hivyo Partey amekana madai hayo.

CHANZO:Reuters
Soma zaidi
Waandamanaji nchini Afrika Kusini wanavamia nyumba hadi nyumba kuwasaka wahamiaji
Morocco yaahidi kujiimarisha zaidi baada ya kutolewa Kombe la Dunia
Benki ya Dunia: Wakenya milioni 2.4 wako hatarini kutumbukia kwenye umaskini
Aliyekuwa Kiongozi Mkuu wa Iran, Ali Khamenei azikwa, huku waombolezaji waapa kulipiza kisasi
Urusi kuisaidia Msumbiji kupambana na ugaidi
Tanzania: Watu 130 wakamatwa kwa kuhamasisha vitendo vya kihalifu
Marekani yashambulia daraja muhimu la reli linalounganisha Iran, China na Urusi
Morocco iko imara kuliko Paraguay: Kocha wa Ufaransa Deschamps
Vifo vya Ebola vyafikia 600 nchini DRC huku maambukizi yakiripotiwa katika jimbo jipya
CCM na ACT-Wazalendo wamaliza mgogoro wa kisiasa Zanzibar
Somalia yapongeza upatanishi wa Uturuki baada ya upinzani kukubali mazungumzo ya katiba
Iran yaionya Marekani baada ya mashambulizi mapya, yasema ni Iran pekee itakayoamua hatima ya Hormuz
Tanzania yanunua zaidi ya tani 28 za dhahabu ili kuongeza akiba ya fedha za kigeni
Vita vya Sudan: Watu 10 wameuawa katika shambulio la droni kwenye sherehe ya harusi
Wafanyakazi wa afya nchini DR Congo wagoma huku vifo vya Ebola vikikaribia 600
Polisi na jeshi la Afrika Kusini wawakamata zaidi ya wachimbaji madini haramu 200
Rais Mnangagwa apitisha sheria ya kumuongezea muda wa kukaa madarakani
Ufaransa yawaondoa wanadiplomasia kutoka Burkina Faso.
Saba Saba: Polisi wapiga marufuku maandamano katika kumbukumbu ya maandamano ya Kenya.
Wakulima wa Uganda wafungua kesi dhidi ya mradi wa bomba la mafuta unaoungwa mkono na Uingereza