| Swahili
ULIMWENGU
2 dk kusoma
Iran “inapaswa kujirekebisha, na haraka,” asema Trump
Rais wa Marekani amesema kuwa maelezo ya Iran kuhusu makubaliano yaliyopendekezwa “hayana uhusiano wowote na ukweli,” na kuwataja Wairani kuwa “watu wasio waaminifu katika mazungumzo.”
Iran “inapaswa kujirekebisha, na haraka,” asema Trump
Rais wa Marekani Donald Trump akizungumza katika Ikulu ya White House. / / Reuters

Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema kuwa toleo la makubaliano yaliyopendekezwa kati ya Marekani na Iran kuhusu kusitisha vita, sio kama lilivyoelezwa na Iran.

Katika ujumbe aliouchapisha kwenye mtandao wake wa kijamii wa Truth Social Ijumaa, Trump alisema kuwa ripoti za vyombo vya habari kuhusu masharti ya waraka wa maelewano kati ya Marekani na Iran zilikuwa si sahihi.

“Masharti ambayo Iran ilivujisha kwa vyombo vya habari potofu (Fake News) hayana uhusiano wowote na masharti yaliyokubaliwa kwa maandishi,” aliandika.

“Walichosema, pamoja na taarifa yao dhaifu na ya kusikitisha kwamba makubaliano yamefikiwa, hakina uhusiano wowote na ukweli. Ni watu wasio waaminifu sana kufanya nao mazungumzo. Kwao, hakuna kitu kama kufanya mazungumzo kwa nia njema. INASHANGAZA! Pia, shambulio lao la ndege zisizo na rubani jana usiku dhidi ya meli za India zilizokuwa zikiondoka katika Mlango-Bahari wa Hormuz, ambalo lilizuiwa, halikubaliki kabisa. Wanapaswa kujirekebisha, na haraka!”

Pande zote zinatofautiana

Shirika rasmi la habari la Iran, Islamic Republic News Agency, hapo awali lilichapisha kile lilichokiita rasimu ya waraka wa maelewano wenye vipengele saba, ambayo ilitofautiana na toleo la makubaliano lililoripotiwa awali na vyombo vya habari vya Marekani.

IRNA ilisema kuwa Iran haitachukua masharti mapya kuhusu nyuklia na itaendelea kuwa na mamlaka kamili juu ya Mlango-Bahari wa Hormuz. Hata hivyo, Shirika la Habari la Axios liliripoti kuwa mfumo wa makubaliano ulijumuisha suala la akiba ya urani iliyorutubishwa ya Iran pamoja na “kufunguliwa mara moja” kwa njia hiyo ya maji bila ya kutoza ushuru.

Kwa mujibu wa ripoti ya Iran, nchi hiyo haitatoa ahadi yoyote ya kuhamisha udhibiti wa Mlango wa Hormuz, njia muhimu ya usafirishaji wa majini ambayo Iran imekuwa ikiidhibiti kwa karibu tangu hatua za mwanzo za mzozo huo.

Badala yake, suala hilo lingeshughulikiwa kupitia mazungumzo na maamuzi ya pamoja kati ya Iran na Oman.

Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ilisema Alhamisi kwamba sehemu kuu ya waraka ya makubaliano ilikuwa imekamilishwa, huku ikiishutumu Mareknai kwa kudhoofisha maendeleo ya mazungumzo kupitia misimamo inayokinzana.

CHANZO:TRT World and Agencies
Soma zaidi
Iran yatishia kushambulia mitambo ya umeme ya nchi za Ghuba iwapo Marekani itashambulia mitambo yake
Nchi 20 za Kiislamu zajadili hatua za pamoja dhidi ya ukiukaji wa Israel katika Msikiti wa Al-Aqsa
Mawaziri wa bara Arabu, Waislamu wakutana Jordan kujadili kwa pamoja Jerusalem Mashariki inayokaliwa
Wahamiaji 70,000 waondoka Hispania huku idadi ya vifo ikiongezeka
Wanafunzi wa Korea Kusini matatani kwa ‘kuvunja’ na kuingia ndani ya kambi ya kijeshi ya Marekani
Wahamiaji wapatao 160 waokolewa baada ya meli yao kuwaka moto
Chama cha soka cha Palestina chaituhumu FIFA kwa kushindwa kuiadhibu Israel
Trump aitaka Iran ichague kati ya makubaliano na kujislamisha
Namna kijana mwenye umri wa miaka 12 mwenye usonji alivyotumia uokaji keki kukabiliana na chuki
Australia yathibitisha vifo vya ndege vinavyotokana na mafua H5
Iran: Hatuna mazungumzo yoyote na Marekani
Mashambulizi ya Israel yaua Wapalestina 12, wakiwemo watoto wawili, huko Gaza
Iran inachukulia kila tishio kutoka kwa wapinzani kuwa "halisi na la kuaminika" : Kaimu Waziri
Trump asitisha shambulio lililopangwa dhidi ya Iran
Hamas yakubali kusalimisha silaha nzito katika 'uamuzi mgumu' kama sehemu ya makubaliano
Makubaliano ya nyuklia ya Marekani na Saudi Arabia yanabadilisha muelekeo Mashariki ya Kati
Taifa la Nauru labadilisha jina, sasa kuitwa Naoero
China yakana taarifa za kusafirisha vifaa vya kurusha makombora Iran
Marekani yaanzisha wimbi jipya la mashambulizi dhidi ya Iran
Watu wasiojulikana waharibu kituo cha hija ya Wakatoliki nchini Bosnia