| Swahili
ULIMWENGU
2 dk kusoma
Iran “inapaswa kujirekebisha, na haraka,” asema Trump
Rais wa Marekani amesema kuwa maelezo ya Iran kuhusu makubaliano yaliyopendekezwa “hayana uhusiano wowote na ukweli,” na kuwataja Wairani kuwa “watu wasio waaminifu katika mazungumzo.”
Iran “inapaswa kujirekebisha, na haraka,” asema Trump
Rais wa Marekani Donald Trump akizungumza katika Ikulu ya White House. / / Reuters

Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema kuwa toleo la makubaliano yaliyopendekezwa kati ya Marekani na Iran kuhusu kusitisha vita, sio kama lilivyoelezwa na Iran.

Katika ujumbe aliouchapisha kwenye mtandao wake wa kijamii wa Truth Social Ijumaa, Trump alisema kuwa ripoti za vyombo vya habari kuhusu masharti ya waraka wa maelewano kati ya Marekani na Iran zilikuwa si sahihi.

“Masharti ambayo Iran ilivujisha kwa vyombo vya habari potofu (Fake News) hayana uhusiano wowote na masharti yaliyokubaliwa kwa maandishi,” aliandika.

“Walichosema, pamoja na taarifa yao dhaifu na ya kusikitisha kwamba makubaliano yamefikiwa, hakina uhusiano wowote na ukweli. Ni watu wasio waaminifu sana kufanya nao mazungumzo. Kwao, hakuna kitu kama kufanya mazungumzo kwa nia njema. INASHANGAZA! Pia, shambulio lao la ndege zisizo na rubani jana usiku dhidi ya meli za India zilizokuwa zikiondoka katika Mlango-Bahari wa Hormuz, ambalo lilizuiwa, halikubaliki kabisa. Wanapaswa kujirekebisha, na haraka!”

Pande zote zinatofautiana

Shirika rasmi la habari la Iran, Islamic Republic News Agency, hapo awali lilichapisha kile lilichokiita rasimu ya waraka wa maelewano wenye vipengele saba, ambayo ilitofautiana na toleo la makubaliano lililoripotiwa awali na vyombo vya habari vya Marekani.

IRNA ilisema kuwa Iran haitachukua masharti mapya kuhusu nyuklia na itaendelea kuwa na mamlaka kamili juu ya Mlango-Bahari wa Hormuz. Hata hivyo, Shirika la Habari la Axios liliripoti kuwa mfumo wa makubaliano ulijumuisha suala la akiba ya urani iliyorutubishwa ya Iran pamoja na “kufunguliwa mara moja” kwa njia hiyo ya maji bila ya kutoza ushuru.

Kwa mujibu wa ripoti ya Iran, nchi hiyo haitatoa ahadi yoyote ya kuhamisha udhibiti wa Mlango wa Hormuz, njia muhimu ya usafirishaji wa majini ambayo Iran imekuwa ikiidhibiti kwa karibu tangu hatua za mwanzo za mzozo huo.

Badala yake, suala hilo lingeshughulikiwa kupitia mazungumzo na maamuzi ya pamoja kati ya Iran na Oman.

Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ilisema Alhamisi kwamba sehemu kuu ya waraka ya makubaliano ilikuwa imekamilishwa, huku ikiishutumu Mareknai kwa kudhoofisha maendeleo ya mazungumzo kupitia misimamo inayokinzana.

CHANZO:TRT World and Agencies
Soma zaidi
Polisi wapekua nyumba ya rais wa zamani, Jair Bolsonaro
Ukraine, Uholanzi zatiliana saini mkataba wa ulinzi wakati wa mkutano wa NATO
Gaza yavunja utawala kabla ya uhamisho wa mamlaka chini ya makubaliano ya kusitisha mapigano
Ufaransa yakumbwa na wizi mwingine mkubwa wa vito vya thamani kutoka jumba la makumbusho
Trump kukutana na Zelenskyy, Sharaa wa Syria wakati wa mkutano wa NATO mjini Ankara
Watu 8 wauawa katika tukio la hivi punde la uhalifu wa  bunduki nchini Marekani.
Maombi yamefanyika kwa ajili ya Khamenei wa Iran katika siku ya pili ya sherehe za mazishi
Sherehe za mazishi ya Ali Khamenei zinaanza nchini Iran huku umati mkubwa ukidai kulipizwa kisasi
Uturuki yakanusha taarifa za kupotosha kuhusu tishio la shambulio wakati wa mkutano wa NATO
Waziri Mkuu wa Moldova ajiuzulu baada ya miezi nane madarakani
Kanisa Katoliki lajitenga na Jumuiya ya Mtakatifu Pius wa 10
Mazungumzo ya nyuklia kati ya Iran na Marekani yamepiga hatua nzuri: Trump
Jinsi urembeshaji wa kitamaduni unavyoweka utambulisho wa Wapalestina hai katika diaspora
Ufaransa yarekodi vifo zaidi ya 1,000 katika siku tano huku wimbi la joto likizidi kupanda
Kisa cha paka Larry na Mawaziri Wakuu wa Uingereza
Huduma za usafirishaji zapungua Mlango Bahari wa Hormuz baada ya mashambulizi ya meli za mizigo
Ajali mbaya ya ndege nchini Ufaransa, uchunguzi waanza
Umoja wa Mataifa unakadiria karibu watu milioni 6.8 waliathiriwa na tetemeko la ardhi la Venezuela
Lebanon, Israel na Marekani watia saini mpango wa makubaliano ya amani
Rais Zelenskyy  wa Ukraine ‘atenga’ siku 40 za kuishambulia Urusi