| Swahili
UTURUKI
1 dk kusoma
Erdogan akutana na timu ya Voliboli ya wanawake ya Uturuki baada ya ubingwa wa Ulaya
“Tumefurahishwa sana kuona matokeo ya uwekezaji wetu mkubwa katika michezo, hasa voliboli,” kiongozi wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amesema.
Erdogan akutana na timu ya Voliboli ya wanawake ya Uturuki baada ya ubingwa wa Ulaya
Erdogan aliipongeza timu hiyo ya wanawake kwa ubingwa wa mashindano ya Ulaya 2026 CEV kwa mara ya pili mfululizo.

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan siku ya Jumanne amekutana na timu ya taifa ya wanawake ya voliboli, ambayo imechukua ubingwa wa Ulaya, na wachezaji wengine waliotuzwa medali katika Ikulu ya rais jijini Ankara.

Erdogan aliipongeza timu hiyo ya wanawake kwa ubingwa wa Ulaya 2026 CEV kwa mara ya pili mfululizo, pamoja na wachezaji wa voliboli wa Uturuki ambao wamepata mafanikio katika mashindano mengine ya kimataifa.

“Tumefurahishwa sana kuona matokeo ya uwekezaji mkubwa katika michezo, hasa voliboli,” alisema.

Akieleza kuhusu mashindano ya Olimpiki ya 2028 Los Angeles, ambapo Uturuki imefuzu tayari, Erdogan alisema “hana shaka” kuwa timu hiyo inaweza kushinda ubingwa wa mashindano hayo.

“Tuna imani, tunajiamini. Mungu akipenda, tutafanikiwa,” aliongeza.

CHANZO:َAA