| swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Ripoti: Ofisi ya Rais Ruto yatumia zaidi ya dola elfu 15 kwa huduma za uchapishaji kwa siku
Ofisi ya Rais wa Jamhuri ya Kenya imetumia zaidi ya dola elfu 15 sawa na shilingi milioni 2 za Kenya kwa siku katika huduma za uchapishaji katika mwaka uliopita wa kifedha.
Ripoti: Ofisi ya Rais Ruto yatumia zaidi ya dola elfu 15 kwa huduma za uchapishaji kwa siku
Bajeti ya uchapishaji iliongezeka kutokana na idadi kubwa ya wageni waliokuwa wakialikwa Ikulu kushiriki mkutano wa Rais. /
3 Septemba 2025

Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Msimamizi wa Bajeti, Bi Margaret Nyakang’o.

Ripoti hiyo, ambayo imebainisha matumizi ya kupindukia na yasiyo ya lazima serikalini, imeonyesha pia kuwa ofisi ya Rais William Ruto ilitumia zaidi ya dola milioni 7 sawa na shilingi bilioni 1 za Kenya kwa ajili ya malipo ya washauri wake, ambao sasa wamefikia 20 chini ya utawala wa Kenya Kwanza.

Licha ya ahadi zilizotolewa za kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ili kuziba pengo la bajeti, ripoti inaonyesha kuwa serikali haina utashi huo.

Huduma hizo za uchapishaji zilihusisha matumizi ya karatasi kwa ajili ya kuchapisha sera za serikali, maagizo ya Rais, matangazo rasmi yaliyotumwa kwa mashirika ya serikali, mikataba ya utendaji, taarifa kwa vyombo vya habari kila baada ya wiki mbili, mawasiliano ya mara kwa mara ya serikali nyakati za dharura, pamoja na huduma nyengine.

Aidha, bajeti ya uchapishaji iliongezeka kutokana na idadi kubwa ya wageni waliokuwa wakialikwa Ikulu kushiriki mikutano na Rais, hali iliyohitaji uchapishaji wa kadi za mialiko kwa kutumia karatasi za ubora wa juu.

Ripoti hii inakuwa wakati ambapo, serikali ya nchi hiyo, iko mbioni katika kunadi sera ya matumizi rafiki ya mazingira ikiwemo kupunguza matumizi ya karatasi.

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi
AU yakanusha tuhuma za Trump kuhusu mauaji ya halaiki Nigeria
Mwigulu Nchemba ateuliwa Waziri Mkuu Tanzania
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti