| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Nigeria yawapata magaidi wanne na hatia kwa mauaji ya kanisani mwaka 2022
Jaji nchini Nigeria amewapata na hatia wanaume wanne katika kesi ya ugaidi kuhusu mauaji katika kanisa 2022.
Nigeria yawapata magaidi wanne na hatia kwa mauaji ya kanisani mwaka 2022
Mahakama nchini Nigeria Juni 3, 2026 imewahukumu wanaume wanne kuuawa kutokana na mauaji ya mwaka 2022 katika kanisa. / Reuters

Jaji nchini Nigeria siku ya Jumatano amewapata na hatia wanaume wanne katika kesi ya ugaidi kuhusu mauaji katika kanisa 2022, huku akimuacha huru mtu wa tano.

Kufyatua risasi na kurusha mabomu katika kanisa la Katoliki la St Francis Xavier mji wa Owo, kusini magharibi mwa jimbo la Ondo, kulisababisha vifo vya zaidi ya watu 40 na wengine 100 kujeruhiwa, kulingana na mwendesha mashtaka.

Jaji Emeka Nwite wa Mahakama Kuu ya Abuja iliwapata na hatia Idris Abdulmalik Omeiza, Al Qasim Idris, Jamiu Abdulmalik na Abdulhaleem Idris ya makosa tisa yaliyowasilishwa chini ya Sheria ya Ugaidi ya 2022 (Kuzuia na Kupinga), ikiwa ni pamoja na kujiunga na kundi la kigaidi hadi kupanga njama na kufanya mauaji.

Walihukumiwa kifungo cha maisha kila mmoja, na kuuawa, ingawa kwa sheria ya Nigeria watu hawauawi.

'Haki imetendeka'

Mshtakiwa wa tano, Momoh Otuho Abubakar, hakupatikana na hatia na kuachiwa huru.

"Haki imetendeka, haki imepatikana kwa waliouawa kikatili," mwendesha mashtaka Ayodeji Adedipe aliwaambia waandishi wa habari.

Wakili wa upande wa washtakiwa Abdullahi Muhammad amesema watakata rufaa ya hukumu hiyo.

CHANZO:TRT Afrika Swahili