| swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Uturuki imetuma “Meli ya Ukarimu” ya 17 yenye msaada wa tani 900 kuelekea Gaza
Uturuki imetuma “Meli ya Ukarimu” ya 17 ikiwa na tani 900 za misaada ya kibinadamu kuelekea Gaza, ikiwa ni sehemu ya juhudi endelevu za misaada baada ya kusitishwa kwa mapigano.
Uturuki imetuma “Meli ya Ukarimu” ya 17 yenye msaada wa tani 900 kuelekea Gaza
"Meli ya 17 ya Ukarimu," ya Uturuki iliyobeba msaada wa Gaza, imeondoka Bandari ya Mersin kuelekea Bandari ya Al Arish ya Misri Oktoba 14, 2025. /
14 Oktoba 2025

Meli hiyo, iliyopakiwa takribani tani 900 za chakula na mahitaji ya watoto wachanga, iliondoka Jumanne katika Bandari ya Kimataifa ya Mersin, kusini mwa Uturuki, kuelekea Bandari ya Al Arish nchini Misri.

Misaada hiyo imepangwa chini ya uratibu wa Idara ya Kudhibiti Majanga na Dharura ya Uturuki (AFAD) kwa ushirikiano na shirika la Hilali Nyekundu ya Misri, vile vile ilijumuisha misaada ya mashirika yasiyo ya kiserikali 17.

Mizigo hiyo ya msaada itapitia katika mpaka wa Karem Abu Salem kupitia Bandari ya Al Arish, bandari iliyo karibu zaidi na Ukanda wa Gaza.

Misaada hiyo, iliyotayarishwa kusaidia wakazi wa Gaza kukidhi mahitaji yao ya msingi, inajumuisha chakula tayari kuliwa, vyakula vya makopo na maziwa ya watoto wachanga.

Wakati wa hafla ya kuaga meli hiyo katika Bandari ya Mersin, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uturuki, Ali Yerlikaya, alisema: “Leo tunasema ‘Meli ya Ukarimu inaelekea Gaza.’ Chombo hiki cha Bahari ya Mediterania kimebeba tani 900 za chakula, vyakula vya makopo na maziwa ya watoto wachanga, na sasa kinaelekea Gaza.”

Tangu kuanza kwa mashambulizi ya mauaji ya halaiki ya Israel dhidi ya Gaza tarehe 7 Oktoba 2023, Uturuki imekuwa ikitoa misaada ya kibinadamu kupitia meli 16 na ndege 14 chini ya uratibu wa AFAD.

Wiki iliyopita, mkataba wa kusitisha mapigano ulifikiwa kama sehemu ya mpango wa Rais wa Marekani Donald Trump wa kumaliza kabisa vita vilivyowaua zaidi ya Wapalestina 67,000 na kuharibu eneo lote la Gaza.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Wanajeshi 20 wa Uturuki wauawa katika ajali ya ndege ya shehena ya kijeshi huko Georgia: wizara
Ndege ya kijeshi ya mizigo ya Uturuki yaanguka mpakani mwa Georgia na Azerbaijan ikiwa na watu 20
Uimarishaji wa Uturuki ni heshima na kumuenzi Ataturk: Erdogan
Uturuki inamkumbuka Ataturk miaka 87 baada ya kufariki
Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki kuzuru Marekani siku ya Jumatatu
Rais Erdogan anatumai Marekani itatimiza ahadi zake kuhusu makubaliano ya ndege za kivita za F-35
Palestina inapongeza amri za kukamatwa dhidi ya maafisa 37 wa Israel kutoka Uturuki kama 'ushindi
Ujumbe wa Erdogan 'Azerbaijan haiko peke yake' ulipelekea ushindi wa Karabakh: Aliyev
Ushindi wa Karabakh wa Azerbaijan kwa amani ya Caucasus: Rais Erdogan
Uturuki yatoa hati ya kukamatwa kwa Waziri Mkuu wa Israel Netanyahu, juu ya mashtaka ya mauaji
Erdogan: Uturuki kuharakisha miradi ya kiulinzi kuimarisha ‘maslahi’ na washirika wa Ulaya
Uturuki kuandaa mazungumzo ya Gaza wiki ijayo kufuatia wasiwasi juu ya usitishaji mapigano – Fidan
Mfumo wa ulimwengu wa sasa unazingatia nguvu zaidi ya haki: Mkurugenzi wa TRT
Israel imeigeuza Gaza kuwa vifusi, inawezaji kuwa haina hatia: Erdogan
Uturuki yakashifu unafiki wa nchi za Magharibi kuhusu Gaza, yatoa wito wa mfumo mpya wa dunia
Hamas haina nuyklia, Israel iko nayo: Erdogan aitaka Berlin ichukue hatua kali dhidi ya Tel Aviv
Erdogan ataka kuona mabadiliko katika uhusiano na EU na ushirikiano wa kikanda alipokutana na Mertz
Ujerumani yatoa wito wa kuunda “ushirikiano wa kimkakati” ili kukabiliana na changamoto za kimataifa
"Marekebisho ya Ulimwengu": Jukwaa la 9 la TRT World kuanza Istanbul likiangazia majadiliano na haki
Erdogan ametangaza washindi wa Tuzo Kuu za Utamaduni na Sanaa za Urais mwaka 2025