Tanzania imeikaribisha Misri kuwekeza katika uendelezaji wa Bandari ya Dar es Salaam na ujenzi wa miundombinu ya Bandari ya Bagamoyo, ikiwemo njia ya reli itakayounganisha Kongani ya Viwanda ya Kwala na Reli ya Kisasa (SGR).
Wito huo umetolewa Julai 18, 2026 wakati Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan alipokutana na mgeni wake Rais wa Misri Abdel Fattah El-Sisi jijini Dar es Salaam ambapo Rais huyo yuko katika ziara ya kitaifa ya siku mbili.
Ushirikiano kati ya nchi hizo mbili unatarajiwa kuongeza kiwango cha uwekezaji na biashara kati ya nchi hizo mbili.
Takwimu zinaonesha Misri inashika nafasi ya nane miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa uwekezaji nchini Tanzania, ikiwa na miradi 61 yenye thamani ya takriban Dola Marekani bilioni 1.5, na kuzalisha zaidi ya ajira 4,000 katika sekta ya nishati, viwanda, kilimo, utalii na huduma.
AFRIKA
1 dk kusoma
Tanzania yaikaribishwa Misri kuwekeza katika miundombinu ya bandari ya Bagamoyo na Dar es Salaam
Ushirikiano kati ya nchi hizo mbili unatarajiwa kuongeza kiwango cha uwekezaji na biashara kati ya nchi hizo mbili.
Soma zaidi










