| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Uturuki inavyopambana kupunguza uvutaji sigara kwa vijana
Wizara ya Afya ya Uturuki imefungua kliniki maamulu kwa ajili ya kusaidia vijana kuacha uvutaji sigara na kuzuia uraibu wa nikotini katika umri mdogo.
Uturuki inavyopambana kupunguza uvutaji sigara kwa vijana
Wizara ya Afya ya Uturuki imefungua kliniki mahususi kusaidia vijana kuacha uvutaji sigara na kuzuia uraibu wa nikotini katika umri mdogo. / َAA

Takriban thuluthi mbili ya wavutaji sigara nchini Uturuki wanaanza kutumia tumbaku kabla ya umri wa miaka 18, huku magonjwa yanayohusiana na tumbaku yakisababisha takriban vifo 100,000 kila mwaka, hivyo kuonesha umuhimu wa kuchukuliwa hatua za haraka.

Wataalamu wa afya wanatahadharisha kwamba umri wa vijana ndio mbaya zaidi wa kuwa na tabia za uraibu kutokana na sababu kadhaa ikiwemo makundi, ushawishi kutoka mitandao ya kijamii, na taarifa potofu kuhusu afya na madhara na upatikanaji rahisi wa bidhaa za nikotini.

Maatumizi ya nikotini katika umri mdogo au ujana yanaweza kuwa na madhara katika ukuaji wa ubongo, hivyo kusababisha matatizo ya muda mrefu.

Matumizi ya tumbaku katika umri mdogo pia yanaweza kusababisha matumizi ya uraibu wa ulevi katika maisha ya baadae.

Kliniki za Wizara ya Afya za kuzuia uvutaji sigara kwa vijana zinalenga kutoa tathmini kwa vijana, ushauri nasaha na matibabu.

Kliniki pia zinatoa msaada wa ushuhuda kwa kuwashirikisha wanasaikolojia wa watoto na vijana, watumishi wa jamii na wabobezi wengine inapolazimika.

Maafisa wa afya wanasema hatua za awali ni muhimu sio tu kwa kuzuia matumizi ya tumbaku bali pia kuzuia utegemezi wa nikotini kuwa uraibu wa muda mrefu na kupunguza athari zake kiafya.

Upanuzi wa kliniki nchi nzima

Kliniki mpya zimeanza kufanya kazi Juni 2026 na hivi sasa zinatoa huduma katika vituo saba katika maeneo ya Agri, Ankara, Bursa, Canakkale, Corum na Kutahya.

Wizara ina mpango wa kupanua mpango huo nchi nzima kwa kuongeza idadi ya vituo na mwishowe kufanya huduma za vijana za kuacha uvutaji sigara kupatinana katika kila mkoa.

Uturuki hivi sasa ina kliniki 1,600 zinazohudumia watu nchi nzima kuanzia Julai 9, 2026.

Wizara pia imeandaa muongozo wa kliniki kwa wataalamu wanaofanya kazi katika vituo vipya.

Soma zaidi
Mashambulizi ya Israel yanatishia usalama wa Syria: Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki
Muswada wa “Uturuki Isiyo na Ugaidi” wafungua hatua muhimu katika kukomesha ugaidi: Erdogan
Mkuu wa mawasiliano wa Uturuki anasema Israel inahujumu juhudi za amani za Gaza
Uturuki inaweka historia kwa kusafirisha treni ya kwanza iliyotengenezwa nchini humo kwenda Afrika
Mkuu wa shirika la ujasusi wa Uturuki akutana na kiongozi wa Hamas kujadili mpango wa amani wa Gaza
Rais wa Uturuki na Mwana Mfalme wa Saudia wajadili usalama wa kikanda na mpango wa amani wa Gaza
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki na Kuwait wajadili yanayojiri katika kanda
Mkuu wa mawasiliano wa Uturuki anasema Israel inahujumu juhudi za kutafuta amani Gaza
Uturuki yalaani mashambulizi ya Israel huko Gaza, ikimtuhumu Netanyahu kwa kuhujumu juhudi za amani
Mpango wa 'Uturuki Isiyo na Ugaidi' kupata msukumo kupitia hatua za bunge: Erdogan
Uturuki na Iraq zasaini makubaliano ya kuongeza matumizi ya bomba la mafuta la Kirkuk-Ceyhan
Uturuki yamkamata gaidi wa FETO aliyekuwa akisakwa kwa jaribio la mwaka 2016 la kumuua Rais Erdogan
Sabiha Gokcen ya Istanbul yaongoza kwa ukuaji wa idadi ya abiria kati ya viwanja vya ndege Ulaya
Uturuki yaimarisha utoaji wa misaada duniani, ikisaidia nchi 85
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Sudan wakutana jijini Ankara
Trump apuuza pingamizi la Netanyahu kuhusu uuzaji wa ndege za kivita za F-35 kwa Uturuki
Erdogan wa Uturuki, Faye wa Senegal wajadili uhusiano, masuala ya dunia
Mwanadiplomasia wa Uturuki Fidan ajadili Kupro, Syria na masuala ya kanda na mkuu wa UN Guterres
Mwanadiplomasia mkuu wa Uturuki Fidan ajadili Cyprus, Syria na masuala ya kikanda na Guterres
Lilikuwa ni jambo la kifahari kuandaa mkutano wa NATO jijini Ankara, asema Erdogan