| Swahili
UTURUKI
1 dk kusoma
Mkutano wa NATO Ankara kuwa 'jukwaa muhimu la kubadilishana mawazo': Erdogan wa Uturuki
Rais Recep Tayyip Erdogan ametoa wito wa kuanzishwa kwa mtandao wa usalama na ulinzi wa muungano wa NATO 'bila masharti'.
Mkutano wa NATO Ankara kuwa 'jukwaa muhimu la kubadilishana mawazo': Erdogan wa Uturuki
Rais Recep Tayyip Erdogan akizungumza katika hafla ya Maspika wa Mabunge ya NATO Istanbul, Juni 29, 2026. / AA

Mkutano wa NATO jijini Ankara Julai 7-8 utakuwa "jukwaa muhimu la kubadilishana mawazo," Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amesema.

Akihutubia hafla ya chakula cha mchana kwa maspika wa mabunge ya NATO jijini Istanbul siku ya Jumatatu, Erdogan alisema Uturuki pamoja na washirika wake wote "wana uwezo wa kukabiliana na mizozo katika kanda" na uwezo wa kutosha ndani ya muungano.

Uturuki inaongeza matumizi yake ya kijeshi na ni miongoni mwa mataifa matano yanayotoa mchango mkubwa kwa shughuli za NATO na operesheni, kwa mujibu wa ahadi zilizotolewa kwenye mkutano wa Hague 2025, aliongeza.

Erdogan anasema kuendeleza uwezo wa NATO na kuimarisha umoja miongoni mwa nchi wanachama imekuwa muhimu zaidi katika mpangilio wa kisasa.

Alitoa wito wa kuanzishwa kwa mtandao wa usalama na ulinzi kwa muungano wote wa NATO "bila masharti", "kutoka Texas hadi Ankara."

Akizungumzia kuhusu vita vya Urusi na Ukraine, Erdogan alisema lazima kupatikane njia ya kutatua mzozo huo ulioanza tangu 2022.

Alieleza kuwa suala la Palestina ni la msingi kwa hali ya taharuki Mashariki ya Kati na amani ya kudumu haiwezi kupatikana kama Israel inaendelea na unyakuzi wa ardhi.