| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Bunge la EALA lapongeza nchi wanachama wa EAC kwa kuandaa CHAN 2024
Pongezi hizo zinakuja baada ya Tanzania, Kenya na Uganda, kuandaa michuano ya CHAN kwa pamoja.
Bunge la EALA lapongeza nchi wanachama wa EAC kwa kuandaa CHAN 2024
Wabunge wa EALA wakiwa kikaoni jijini Arusha, Tanzania./Picha:Wengine
8 Oktoba 2025

Wajumbe la Bunge la Afrika Mashariki (EALA) linalokutana jijini Arusha, Tanzania limepitisha azimio la kupongeza baadhi ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kuandaa kwa mafanikio mashindano ya CHAN 2024.

Kulingana na wajumbe hao, mafanikio hayo ni ishara ya umoja wa kikanda na weledi wa kimichezo ndani ya jumuiya hiyo yenye nchi wanachama nane.

Pongezi hizo zinakuja baada ya Tanzania, Kenya na Uganda, kuandaa michuano ya CHAN kwa pamoja.

Azimio hilo, lililowekwa mezani kwa kutumia ibara 49(2)(d), 59(1), 119(a) and (h) na sheria ya uanzishwaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, uliletwa bungeni siku ya Oktoba 7, 2025 na Falhada Dekow Iman kutoka Kenya, huku likiungwa mkono na Clément Musangabatware wa Rwanda.

Kulingana na azimio hilo, nchini ya kifungu 119, nchi wanachama zimejitolea kushirikiana katika kukuza michezo na shughuli za kitamaduni, kama nyenzo ya kukuza utambulisho wa jumuiya hiyo.

Mwezi Agost 2025, Tanzania, Kenya na Uganda, ziliandaa kwa pamoja michuano ya CHAN 2024, ambayo ni maalumu kwa wachezaji wanaoshiriki ligi za ndani.

Wiki kadhaa baadaye, Rwanda iliandaa michuano ya kimataifa ya mbio za baiskeli, zilizofanyika  kutoka Septemba 21 hadi 28, 2025.

"Nchi zetu zimeonesha, sio tu uwezo wake wa kuandaa michuano yenye hadhi ya kimataifa, bali utajiri wa kitamaduni, uzuri asilia na ukarimu wa watu wa Afrika Mashariki,” alisema Iman.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi
AU yakanusha tuhuma za Trump kuhusu mauaji ya halaiki Nigeria
Mwigulu Nchemba ateuliwa Waziri Mkuu Tanzania
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti