Tume ya Umoja wa Ulaya imesema kuwa bidhaa Uturuki zitawekewa nembo ya umoja huo, chini ya mkakati wa viwanda wa wenye kutoa fursa ya ruzuku.
Hatua hiyo, inadhihirisha utayari wa Umoja wa Ulaya wa kufanya biashara kwa ukaribu na Uturuki.
Maofisa wanasema kuwa, mpango huo unalenga kuunga mkono uzalishaji wa bidhaa ndani ya Umoja wa Ulaya na kupambana na ushindani usiokuwa na uwiano.
Viwanda mbalimbali barani Ulaya, hususani kwenye sekta ya teknolojia, ujenzi na kadhalika, vimekumbana na hali kama hiyo kutoka kwa wazalishaji wa kichina.
Kupitia mkakati huo, Umoja wa Ulaya unalenga kutumia mikakati ya manunuzi ya umma, ruzuku na zabuni ili kuongeza mahijati ya bidhaa za kimkakati zilizotengenezwa Ulaya.
Umoja wa Ulaya kuimarisha biashara ya magari ya Uturuki
Umoja wa Ulaya na Uturuki zinakutana katika Ushuru wa Forodha, huku mpango huo ukitoa ufafanuzi na uhakika kwa makampuni ya Kituruki yaliyo Ulaya pamoja na bidhaa wanazozalisha.
Hata hivyo, kwa sasa makampuni ya Uturuki hayatokuwa na uwezo wa kushiriki moja kwa moja kwenye zabuni ndani ya Umoja wa Ulaya, ikiwemo ujenzi wa shule, hospitali, kulingana na Msemaji wa Tume ya Umoja wa Ulaya.
Licha ya hayo, bidhaa mbalimbali kama vile saruji na mabati zinunuliwazo na makampuni ya Ulaya kutoka Uturuki, bado zinaweza kutumika katika miradi yenye kufadhiliwa kupitia miradi ya manunuzi ya Umoja wa Ulaya.
“Kwa sasa, Uturuki itapata hadhi sawa kama ilivyo kwa wanachama wengine wa Umoja wa Ulaya,” alisema msemaji huyo.

















