DRC na Rwanda zakubali hatua za utekelezaji wa makubaliano ya amani yaliyokwama
Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa pande hizo mbili kukutana tangu Marekani kuweikea vikwazo jeshi la Rwanda na maafisa wanne wa jeshi hilo Machi 2.
Marekani iliwakaribisha wawakilishi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Rwanda mjini Washington siku ya Jumanne na Jumatano, katika mazungumzo ya mchakato wa amani uliokwama mashariki mwa DRC.
Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa pande hizo mbili kukutana tangu Marekani kuliwekea vikwazo jeshi la Rwanda na maafisa wanne wa jeshi hilo Machi 2.
Marekani imeilaumu Rwanda kwa kuunga mkono kundi la waasi la M23 ambalo linaendeleza ghasia mashariki mwa Congo. Madai ambayo Rwanda inayakanusha.
M23 ilifanya jitihada za kusogea mbele mashariki mwa Congo Januari 2025 na bado ina maeneo makubwa.
DRC na Rwanda "zilikubaliana na hatua zilizoratibiwa ili kupunguza mvutano na kuendeleza maendeleo," kulingana na taarifa ya pamoja ya Marekani, DRC na Rwanda iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje siku ya Jumatano.
"Juhudi hizi ni pamoja na dhamira ya pande zote kwa hatua mahususi za kuunga mkono mamlaka na uadilifu wa eneo la kila mmoja, utenganishaji uliopangwa wa majeshi/kuondoa hatua za ulinzi na Rwanda katika maeneo yaliyoainishwa katika eneo la DRC, juhudi za muda na zilizoimarishwa za DRC ili kutokomeza FDLR, na ulinzi wa raia wote."
Kundi la FDLR lilianzishwa na Wahutu waliokimbia Rwanda baada ya kushiriki katika mauaji ya halaiki ya mwaka 1994 ambayo yaliua karibu Watutsi milioni moja na Wahutu wenye msimamo wa wastani. M23 inasema inapigania kulinda jamii za kabila la Watutsi mashariki mwa DRC.
Rwanda na DRC zilitia saini mkataba wa amani mjini Washington mwezi Disemba kama sehemu ya msukumo wa Rais wa Marekani Donald Trump wa kuleta amani na kuvutia mabilioni ya dola katika uwekezaji wa nchi za Magharibi.
Siku chache baada ya sherehe hiyo, waasi wa M23 waliingia katika mji wa mashariki wa Congo wa Uvira, karibu na mpaka wa Burundi, katika ongezeko kubwa la mapigano katika miezi kadhaa.
Baadaye walijiondoa chini ya shinikizo la Marekani. Marekani imesema kuendelea kuwepo kwa waasi karibu na mpaka wa Burundi "kuna hatari ya kuzidisha mzozo huo hadi kuwa vita vya kikanda."