Wanafunzi tisa wanaoshtumiwa kupanga njama na kuchoma moto uliosababisha vifo vya wasichana 16 katika shule moja katikati mwa Kenya wamefikishwa mahakamani siku ya Jumanne.
Wachunguzi wameomba muda zaidi wa kufanya uchunguzi wa ajali hiyo ya moto.
Mahakama kuu ya mjini Naivasha, kilomita 90 magharibi mwa mji mkuu wa Nairobi, ilisema itatoa hukumu siku ya Jumatano iwapo wasichana hao watazuiliwa kwa mwezi mmoja huku uchunguzi ukiendelea.
Moto huo wa Mei 28 ulichoma bweni la shule ya Utumishi Academy lililokuwa na wanafunzi 202.
Kuchoma godoro
Wasichana wanaoshutumiwa wamekuwa kituo cha polisi kwa siku tano, ambapo uchunguzi ulibaini moto ulianzishwa kwa kuchoma godoro karibu na mlango wa bweni kwa kutumia kiberiti na mafuta ya taa. Chanzo cha kufanya hivyo hakijabainika kufikia sasa.
Matokeo ya vipimo vya DNA kutambua miili iliyochomwa moto yanatarajiwa siku ya Jumatano.
Picha za CCTV zilizopatikana zinaonesha wanafunzi sita wakianzisha moto, kisha wanafunzi wanaamka na kuanza kukimbia, kusababisha 79 kujeruhiwa.
Moto katika shule
Moto katika shule za nchini Kenya, ambapo madarasa na mabweni yanakuwa yamejaa wanafunzi kupita kiasi na vifaa vya zimamoto huwa havifiki kwa wakati.
Ajali mbaya zaidi ya moto ilitokea 2001, ambapo wanafunzi 67 waliuawa katika Kaunti ya Machakos, na ajali nyingine ya hivi karibuni ilikuwa 2024, ambapo watoto 21 waliuawa katika Kaunti ya Nyeri.
Pia kumekuwa na matukio ya wanafunzi kuchoma moto shule kwa sababu za utovu wa nidhamu.


















