Israel yawaua takriban watu tisa Lebanon, na kukiuka makubaliano ya kusitisha mapigano
"Israel ilianzisha mashambulizi ya anga kusini mwa Lebanon, na kuua watu tisa na kuwajeruhi wengine watatu huku kukiwa na usitishaji wa mapigano uliokiukwa na Tel Aviv, kulingana na Wizara ya Afya ya Lebanon.
Mashambulizi hayo yalilenga kijiji cha Haris, ambapo watano waliuawa na wawili kujeruhiwa, na kijiji cha Tallous, ambapo watu wanne walipoteza maisha na mtu mmoja kujeruhiwa.
Israel imekiuka usitishaji mapigano na Lebanon karibu mara "100" tangu makubaliano hayo kuanza kutekelezwa wiki iliyopita, kulingana na CNN."
Rais Recep Tayyip Erdogan alitangaza kuwa Uturuki inafuatilia kwa karibu mapigano mapya kati ya utawala wa Bashar al Assad na makundi ya upinzani yenye silaha nchini Syria.
Amesisitiza kuwa Ankara inachukua hatua zinazohitajika kukabiliana na mzozo huo.
Rais Erdogan alisisitiza kujitolea kwa Uturuki kwa utulivu wa kikanda, akisema, ""Tunabaki tayari kufanya chochote tunachopaswa kuzima moto katika eneo letu."
Mkurugenzi mteule wa Shirika la WHO Afrika kuzikwa leo
Daktari Faustine Engelbert Ndugulile aliyekuwa pia mbunge wa Kigamboni nchini Tanzania. Mwili wake unatarajiwa kuzikwa leo tarehe 03 ya mwezi Disemba 2024 katika makaburi ya Mwongozo Wilayani Kigamboni Jijini Dar es Salaam. Alishinda nafasi ya ukurugenzi wa WHO, Kanda ya Afrika, mnamo Agosti 2024. Alitarajiwa kuanza rasmi wadhifa huo mwezi Februari 2025.
Zelenskyy: Ukraine inataka kurudisha tena kutoka Urusi kupitia diplomasia
"Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy alisema kuwa Kiev inalenga kurejesha maeneo yaliyo chini ya udhibiti wa Urusi, ikiwa ni pamoja na Crimea, kupitia njia za kidiplomasia.
""Jeshi letu halina nguvu ya kurudisha baadhi ya maeneo, kama Crimea. Hiyo ni kweli. Lazima tutafute suluhu za kidiplomasia,” Zelenskyy alisema wakati wa mahojiano na Kyodo News ya Japan.
Alisisitiza kwamba mazungumzo ya kidiplomasia yataendelea tu wakati Ukraine itahisi kuwa na "nguvu ya kutosha"" kuzuia hatua zaidi za kijeshi za Urusi, kuhakikisha suluhu thabiti kwa mzozo huo."
