25 Desemba 2024
Ili kuelewa, lazima turudi mwaka 1492. Mwaka ambao Granada, ngome ya mwisho ya Kiislamu nchini Hispania, ilianguka. Wakati majeshi ya Kikristo ya Mfalme Ferdinand na Malkia Isabella yalipoteka mji huo. Iliashiria mwisho wa karibu karne nane za utawala wa Kiislamu.
Mwanzoni, Waislamu nchini Hispania waliruhusiwa kubaki chini ya masharti fulani, lakini uvumilivu huu haukudumu kwa muda mrefu. Mwaka 1502, amri ililazimisha Waislamu kuingia katika dini ya Ukristo au kuondoka Hispania. Wale waliobaki walijulikana kama Wamorisco, na wengi waliendelea kufanya ibada za Kiislamu kwa siri.
