| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Upinzani Tanzania wasema mamia wameuawa, UN yataka uchunguzi ufanyike
Waziri wa Mambo ya Nje Mahmoud Thabit Kombo, amekanusha madai ya upinzani ya kwamba mamia wameuawa.
Upinzani Tanzania wasema mamia wameuawa, UN yataka uchunguzi ufanyike
Waandamanaji nchini Tanzania wamejitokeza kupinga shughuli za uchaguzi. / / Reuters
31 Oktoba 2025

Chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania CHADEMA, kimesema siku ya Ijumaa kwamba mamia ya watu wameuawa katika maandamano ya kupinga shughuli za uchaguzi zilizofanyika wiki hii, huku Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, akitoa wito wa kufanyika uchunguzi kuhusu madai ya serikali kutumia nguvu za kupita kiasi dhidi ya waandamanaji.

Aidha, Shirika la Umoja wa Mataifa limesema taarifa za kuaminika zinaonyesha kwamba takriban watu 10 wameuawa katika maandamano yaliyotokea katika miji mitatu, ikiwa ni mara ya kwanza kwa taasisi ya kimataifa kutoa idadi ya makadirio ya vifo tangu uchaguzi uanze.

Hata hivyo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Mahmoud Thabit Kombo alipohojiwa na shirika la habari la Reuters, amesema idadi ya vifo iliyotolewa na upinzani si ya kweli, akisisitiza ya kwamba serikali bado haiwezi kuthibitisha idadi ya watu waliouawa. Waziri huyo pia alikanusha madai kwamba maafisa wa usalama wametumia nguvu kupita kiasi.

CHANZO:Reuters
Soma zaidi
Afrika Kusini yaomba utulivu kufuatia maandamano dhidi ya kusimikwa kwa 'Igwe' wa Nigeria
Rwanda ‘yahofia’ operesheni za DRC dhidi ya kikundi cha FDLR
Kenya yalipa ada ya Dola milioni 30 ya uenyeji wa AFCON 2027
Hasara ya mamilioni kufuatia ubomoaji katika soko kubwa zaidi la wazi la Gikomba Nairobi
Shabiki maarufu ‘Lumumba Vea’ akosa viza ya  kwenda kuishangilia DRC dhidi ya Jamaica
Mamlaka ya uchukuzi Kenya yazindua ukaguzi wa lazima wa afya kwa madereva ili kupunguza ajali
Tanzania yahimiza matumizi ya AI kuimarisha mtangamano na maendeleo EAC
Kundi lenye silaha limewaua watu wasiopungua 20 Jimbo la Plateau nchini Nigeria
Wafungwa wasiopungua 11 wafariki kutokana na mlipuko wa kipindupindu katika jela DRC
Kagame awaamuru maafisa waandamizi wa serikali 'kusimama' wakati wa hotuba yake
Wadukuzi wadukua maombi ya kazi 450,000 nchini Afrika Kusini
Rais wa Misri asema ni Trump pekee anaweza kusimamisha vita, aonya kupanda zaidi kwa bei ya mafuta
Togo yatoa uzoefu wa kupambana na magonjwa yasiyopewa kipaumbele
Watu 15 wamefariki katika ajali ya barabarani mkoa wa kati Kenya
Mahakama kuu ya Jamhuri ya Congo imethibitisha ushindi wa Sassou Nguesso kwa awamu ya tano
Rwanda, Burundi wanagombana juu ya juhudi za rais wa zamani wa Senegal Sall kuongoza UN
Vifo kutokana na mafuriko nchini Kenya vyaongezeka hadi 108, polisi wasema
Majenerali wakuu wa Uganda wazuiliwa kwa madai ya ufisadi: ripoti
Eswatini yamrudisha nyumbani mwananchi wa Cambodia aliyefukuzwa kutoka Marekani
Waasi waanza kuondoka katika vijiji vya DRC ili kuhimiza amani