Rais wa Togo Faure Essozimna Gnassingbe / Photo: AFP

Togo ilisema Alhamisi kwamba imetoa dola milioni 1.5 kusaidia Uturuki kutokana na matetemeko makubwa ya ardhi yaliyokumba eneo la kusini mwa nchi hiyo mnamo Februari 6.

"Togo inajiunga na uhamasishaji wa kimataifa" kwa kutoa "mchango huu wa kuponya majeraha na kushiriki katika ujenzi upya" wa Uturuki baada ya matetemeko mawili ya ardhi yaliyoua zaidi ya watu 50,000, ilisema tovuti ya Jamhuri ya Togo.

Ubalozi wa Uturuki uliishukuru nchi hiyo ya Afrika Magharibi kwa "mshikamano na urafiki ambao umeonyesha."

Pia ilisema kuwa mnamo Machi 21, ubalozi wa Togo huko Ankara ulishiriki katika operesheni ya upandaji miti pamoja na viongozi na watu wa Uturuki.

Operesheni hiyo inahusisha uundaji wa "Msitu wa Kumbukumbu ya Mashujaa wa Tetemeko la Februari 6" katika mikoa 81 nchini humo kwa ajili ya kuwaenzi wahanga wa tetemeko la ardhi.

AA