Watu 23 wafariki kufuatia mvua kubwa iliyosababisha maporomoko ya udongo katika kisiwa cha Sulawesi, Indonesia, / Picha: AA

Zaidi ya vijiji 100 vilikuwa vikichimba dhahabu Jumapili katika eneo la milima la Bone Bolango katika mkoa wa Gorontalo pindi tani za udongo zilipoporomoka na kuzika kambi zao za muda.

Shughuli ya uokozi ilisitishwa Jumatano jioni kutokana na mvua kubwa, amesema Heriyanto, kiongozi wa ofisi ya uokozi ya mkoa. Vikosi vya uokoaji bado havijaweza kuwapata wanaotafutwa, amesema.

Wakala wa Taifa wa Utafutaji na Uokoaji imesema Jumatano kwamba wanakijiji 92 walifanikiwa kukimbia maporomoko hayo.

Baada yao walitolewa kutoka kwenye udongo na waokoaji, ikiwemo 18 waliojeruhiwa.

Taarifa hiyo imeongeza kusema, watu 23 waliokolewa, akiwemo mtoto wa miaka mine, huku 30 wengine wakiendelea kutafutwa.

Zaidi ya maafisa 1,000, wakiwemo wanajeshi, wamepelekwa kusaidia katika utafutaji, amesema Edy Prakoso, mkurugenzi wa operesheni kutoka wakala hiyo.

Amesema vikosi vya anga vya Indonesia itatuma helikopta kuharakisha shughuli za uokozi, ambazo zimezuiwa na mvua kubwa na mmomonyoko wa ardhi.

Uchimbaji usio rasmi unafanyika sana nchini Indonesia, ukitoa ajira kwa maelfu ya raia wa nchi hiyo ambao wanafanya kazi katika mazingira magumu na hata kuhatarisha maisha.

TRT Afrika