Waziri wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amewajulia hali majeruhi 10 wanaoendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Wilaya Temeke.Picha/Wizara ya Sanaa na Utamaduni Tanzania / Photo: TRT World

Katika mkanyagano uliotokea kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam, Tanzania Jumapili wakati wa mchezo wa kwanza wa fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika, CAF, kati ya Yanga na USM Algiers jijini Dar es Salaam, mtu mmoja alipoteza maisha.

Tukio hilo lilitokea baada ya mashabiki kuvunja lango moja la kuingilia na kuwalazimu kuingia uwanjani kushuhudia mechi hiyo ya kihistoria.

Licha ya maafa hayo, mchezo uliendelea, na USM Alger kuwafunga wenyeji Tanzania kwa mabao 2-1.picha/Reuters

Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya wa Tanzania, aeleza kuwa tukio hilo lilitokea wakati umati wa watu ulipojaribu kuingia uwanjani kabla ya mechi kati ya vigogo wawili wa soka barani Afrika. Watu 30 zaidi waliripotiwa kuwa na majeraha madogo, huku wengine kumi wakisemekana kujeruhiwa vibaya.

Majeruhi katika hospitali ya Temeke.Picha/Reuters

“Timu ya wataalam wa Huduma za Dharura wa Hospitali ya Taifa Muhimbili tayari wamewasiliana na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Temeke, na wako tayari kuwapokea na kuwahudumia majeruhi ambao watahitaji matibabu zaidi,” aliandika Waziri Ummy kwenye akaunti yake ya Twitter.

Licha ya maafa hayo, mchezo uliendelea, na USM Alger kuwafunga wenyeji wa Tanzania, Yanga kwa mabao 2-1.

TRT Afrika